Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Spika, ninapenda kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nipende kupongeza juhudi kubwa za Waziri na Naibu Waziri kwa kazi nzuri na ari mliyonayo katika kuhakikisha nchi yetu inaondokana na giza.

Mheshimiwa Spika, nishauri Serikali ilipe fidia kwa wananchi ambao wanapitiwa na miradi ya umeme ili wawe marafiki wa miradi hiyo na waweze kuilinda.

Mheshimiwa Spika, niongelee suala la fidia kwa wanachi wa Mkoa wa Pwani, Kibaha eneo la Kiluvya, Mpiji, Mikongeni na Chalinze. Niombe Serikali ikutane na wanachi hawa kuwapa moyo na kuwaeleza kinachoendelea. Tathmini imefanyika miaka mingi ikifuatiwa na katazo la kutoendelea na shughuli yoyote katika eneo hilo. Hii imewapa umaskini wananchi hao kwani nyumba zao zimechakaa na kuanguka lakini hawana uwezo wa kujenga kwa hili katazo.

Mheshimiwa Spika, ninajua mpango wa usambazaji na uuzaji wa umeme ni wa TANESCO, naona si vyema kulitwisha hili shirika shughuli zote.

Mheshimiwa Spika, nishauri kupunguza urasimu wa kulipa waathirika wa hitilafu za umeme. Kumekuwa na shida pale iwapo hitilafu inatokea, ulipaji wake umekuwa wa shida.

Mheshimiwa Spika, nishauri Serikali juu ya utaratibu wa kuunga umeme kutoka kwenye nguzo ambayo mtu amenunua bila yule anayeungiwa kurudisha angalau nusu hasara kwa aliyeweka nguzo. Mfano mtu amelipia nguzo tano na kuungiwa umeme, kazi ambayo ingefanywa na TANESCO au mteja huyo ambaye wanaenda kumuungia wanaenda kuchukua kwenye nguzo za mteja ambaye alinunua bila hata ridhaa yake, hii siyo nzuri sana.