Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Janet Zebedayo Mbene

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ileje

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. JANET Z. MBENE: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa nafasi ya kuchangia hotuba hii. Najiunga na Waheshimiwa Wabunge wote waliompongeza sana, Mheshimiwa Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani, Mbunge Chato na watendaji wote wa Wizara yake kwa usikivu, ushirikiano, weledi, ufanisi anaoutumia kutekeleza majukumu yake kwa bidii sana. Kwa kweli tunamwombea heri na afya njema katika kutekeleza majukumu yake.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Ileje katika Mkoa wa Songwe imekua mfaidika mkubwa wa REA awamu zote. Ileje ni Wilaya ambayo imekuwa nyuma kwenye eneo la miundombinu ya aina zote, kwa hiyo kupata umeme kutasaidia sana katika kuchochea maendeleo kiuchumi katika Wilaya hii.

Mheshimiwa Spika, Awamu ya I na II aliacha vijiji vingi bila kuwekewa miundombinu ya umeme, ni mahali ambako laini kubwa imepita lakini watu hawajaunganishiwa umeme.

Mheshimiwa Spika, kati ya vijiji 71 vipo vijiji 24 ambavyo bado havina umeme. Ninaviorodhesha hapa kwa hatua za Mheshimiwa Waziri na watendaji wake.

Mheshimiwa Spika,

Na. Kata Na. ya Vijiji Kijiji
1. Bubigu 1 Mabula
2. Chitete 2 Chitete
3. Mbebe 3 Shinji
4. Ibaba 4 Shuba
5. Hale 5 Hega & Iwala
6. Humba 7 Yenzebwe na Nkanka
7. Ndola 8 Ibezya
8. Malangali 9 Chembe & Bulanga
9. Kalembo 11&12 Mbagala & Ibandi
10. Ikinga 13 & 14 Ibeta & Bwipa (shida kubwa)
11. Ngulilo 15, 16 & 17 Ngulilo, Shiringa & Ndapwa
12. Ngulugulu 18, 19 & 20 Chikumbulu, Kisyesye & Bujura
13. Lubanda 21 Mbembati
14. Luswisi 22 & 23 Makoga & Chibila

Mheshimiwa Spika, ninaomba sana Waziri atusaidie kwa hili.

Mheshimiwa Spika, ninaunga mkono hoja.