Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na wataalamu wote wa Wizara ya Nishati.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kazi nzuri inayoendelea, Jimbo la Mbeya Vijijini ambalo kwa kiasi kikubwa vijiji vyake vinalizunguka Jiji la Mbeya bado kuna kata tatu na Vijiji hakuna umeme.

Mheshimiwa Spika, naomba Wizara iharakishe kuwa inapeleka umeme kwenye Vijiji vya Kata ya Maendeleo, Itawa na Kata ya Shizuri, ikiwa na vijiji vingine 42 ambavyo bado havijafikiwa na umeme. Kutokana na uchumi mzuri wa maeneo hayo kutakuwa na manufaa mapana kwa taifa letu na hata kuongeza kipato kwa Shirika la TANESCO.

Mheshimiwa Spika, Kutokana na faida za umeme unaotokana na jotoardhi, napendekeza pia Serikali iweke msukumo mkubwa wa upatikanaji wa umeme wa chanzo hiki cha jotoardhi ambao unategemea kuongeza MW 200.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.