Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kupata nafasi hii ili niweze kuchangia kwa maandishi. Kwanza natoa pongezi kwa Mheshimiwa Rais, Mheshimiwa Waziri na Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kazi nzuri wanayoifanya ndani ya Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, Kuhusu Mradi wa Umeme; Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III). Natoa pongezi kwa jitihada ya Serikali ya malengo ya June 2020 kufikia Vijiji 10,278 na kufikia June 2021 Vijiji vyote vitakuwa na umeme.

Mheshimiwa Spika, vijiji vingi Mkoa wa Morogoro katika Wilaya saba za Morogoro Vijijini, Mvomero, Gairo, Kilombero, Ulanga na Malinyi havijafikiwa na umeme, umeme umefika kwenye centers tu, nazo ni nyumba chache. Naomba umeme Awamu hii ya Tatu vijiji hivi kwenye Wilaya hizi vipatiwe umeme (Mpaka June 2020).

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Kujazilizia Umeme. Kuna Vitongoji vilivyorukwa kama Kimamba D Wilaya ya Kilosa, Vitongoji vya Mtego wa Simba, ikiwemo Chekeleni (karibu na Mikese Fulwe) ambavyo vimerukwa na umeme. Natanguliza shukrani kwa Naibu Waziri kwa sababu ulifika na kuwapatia umeme wananchi wa Kimamba A.

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana, naomba umeme kwa vitongoji vilivyorukwa vya Kimamba A. Mheshimiwa Naibu Waziri alifika Mtego wa Simba (Morogoro Vijijini), nashukuru umeme wamepata, ila ziliwekwa transformer mbili sasa kwenye Kitongoji cha Zahanati ambapo kuna transformer ya pili na nguzo tayari zipo; ni muda mrefu sasa karibu mwaka mzima umepita.

Mheshimiwa Spika, tunaomba umeme kwa hivyo vitongoji vilivyorukwa (kwenye mradi wa kujazilizia).

Mheshimiwa Spika, natoa pongezi pia kwa kupeleka gesi asilia majumbani, gesi itakuwa bei ya chini. Mheshimiwa Waziri kuna Mkakati gani wa kufikisha gesi hii kwenye Miji ya Kibaha (Mkoa wa Pwani) na Mji wa Morogoro (Mkoa wa Morogoro)?

Mheshimiwa Spika, Kuhusu Mradi wa Umeme Mto Rufiji. Natoa pongezi kwa Serikali kwa mradi huu, Serikali tusonge mbele kwani tunahitaji umeme mwingi kwa mambo mbalimbali. Jambo lingine muhimu, miundombinu (barabara) za kufikia mradi zitengenezwe kwa wakati. Naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.