Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Spika, pamoja na jitihada nyingi anazofanya Waziri Kalemani katika kuhakikisha kwamba Tanzania yote inawaka umeme ifikapo 2021 bado jitihada hizi zinakwamishwa na baadhi ya watendaji na wakandarasi. Mawaziri wa Wizara hii wameongea mara nyingi kuwa umeme ukifika kwenye kijiji chochote utafika kila taasisi, kitongoji, lakini kinachofanyika Tanzania hii ni tofauti na kauli za Mawaziri. Katika Wilaya ya Karatu Vijiji vya Huduma, Khusumay, Kauam, Rhotia, Losetete umeme haujaenda kwenye vitongoji bali umeishia kwenye centers za vijiji wananchi wanalalamika sana kwani imeme haujafika kwenye vitongoji.

Mheshimiwa Spika, tatizo hili limesababishwa wa timu za survey ambazo hazikuwasilishwa viongozi wa wananchi. Timu hii maeneo mengine walikwenda hata siku za jumapili na walifanya wenyewe bila kushirikisha viongozi wa wananchi. Niishauri Serikali itoe maelekezo ya kutosha ili survey inapofanyika viongozi wa wananchi washirikishwe ili maeneo yote yafanikiwe.

Mheshimiwa Spika, leo ni mwezi wa tano mwishoni na bado katika Wilaya ya Karatu, Vijiji vya Bugeu, Ayalaliyo, Endanyawe, Kambifairu, Umbang Laja, Quvus. Lositete, Endalals, Bawakta, Mangola Juu pamoja vitongoji vyake bado umeme haujafika. Wananchi wameshajiandaa katika maeneo hayo na wanasubiri wakandarasi. Niombe Waziri uwaelekeze wakandarasi ili wakamilishe kazi hiyo.

Mheshimiwa Spika, nimshukuru sana Waziri, Dkt. Kalemani kwa kutoa transformer tisa ili kuunga visima tisa vya maji kwenye umeme. Kwa niaba ya wananchi wanaotumia visima hivyo nimshukuru sana Waziri. Hata hivyo, nimuombe Waziri afuatilie transformer moja ambayo haijafungwa katika kisima cha Endamavamek, kijiji hiki kiliombewa transformers mbili lakini imefungwa moja tu.