Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Spika, umeme ni nishati muhimu sana na bila umeme wa uhakika tusitarajie Tanzania ya Viwanda wala maendeleo ya kasi. Kwa bahati nzuri sana Tanzania imebarikiwa kuwa na vyanzo vingi sana ikiwemo upepo, makaa ya mawe, gesi asilia na maji. Tunatambua kuwa umeme wa maji ndio ulio na bei rahisi zaidi, ila angalizo la chanzo cha maji ni mabadiliko ya tabianchi.

Inashangaza sana kuona tumeshadadia mradi wa Stiegler’s Gorge bila kuchambua kwa kina uwezo wake (sustainability). Ni lazima tujiulize maswali yafuatayo; je, baada ya miaka mitano na kwa kuzingatia mabadiliko ya tabianchi tutakuwa na maji toshelezi? Hasa ikizingatiwa mvua ndicho chanzo kikuu? Swali la pili, je, athari za kimazingira zimezingatiwaje, hasa kuzingatia ukatwaji mkubwa wa miti?

Mheshimiwa Spika, pamoja na hatua mbalimbai zilizofikiwa kwa mradi huu na kwa kuwa kufanya kosa si kosa bali kurudia kosa, naomba kwa heshima kabisa Serikali ibadili msimamo wake na kuacha kabisa mradi huu ambao athari zake ni kubwa kuliko faida.

Mheshimiwa Spika, kwa muda mrefu nimehoji sababu ya wateja wa umeme kulipia nguzo wakati nguzo hizo zinakuwa mali ya TANESCO? Kwa nini wakati tuna simu za Tanzania Postal & Telecommunications hatukulipia nguzo? Sasa ni sababu zipi zinafanya aliyewahi na kununua nguzo 10 wale wateja wapya watakaotumia nguzo zangu wasinilipe fidia? Wao watalipa service charges tu?

Mheshimiwa Spika, umeme wa REA ni muhimu sana hivyo, tunaomba REA III iongezwe kasi ili vijiji navyo viweze kuendelea na kupunguza kasi ya vijana kuhamia mijini.