Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE: Mheshimiwa Spika, nilizungumza juu ya hoja hii, lakini muda wa dakika tano ni mdogo sana. Hivyo nina jambo la pili ambalo ni kuhusu ubora wa mafuta ya petroli na dizeli hapa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, katika Bunge la 10, Bunge lilichukua hatua ya pekee ya kuzuia wenye vituo vya mafuta kuchakachua mafuta ya petroli na dizeli kwa kuichanganya petrol + kerosene na diesel + Kerosene. Lengo la wafanyabiashara ni kupata faida kubwa sana. Hivyo, Bunge likapandisha bei ya kerosene iwe karibu sawa na diesel au petrol.

Mheshimiwa Spika, kwa muda wa miaka mitano sasa tatizo la kuchakachua mafuta ya petrol na diesel limerudi upya. Takriban vituo vyote vya mafuta leo katika Miji ya Mwanga, Moshi, Arusha, Dodoma, Dar-es-Salaam, Morogoro, Singida, wanauza mafuta yaliyochakachuliwa. Yaelekea kuwa, wafanyabiashara wanaoleta mafuta ya taa kwa bei rahisi kutoka nje (bila kodi) na kuyasambaza nchi nzima. Nchi yetu inapata hasara kubwa sana kwa kutumia mafuta ya kuchakachua, yanaharibu magari, pump, mitambo na viwanda.

Mheshimiwa Spika, haya yote yanatokea na EWURA wapo. EWURA walishindwa kazi ndiyo maana Bunge likachukua hatua. Sasa mafuta yanachakachuliwa sana, huu ni wakati wajue kuwa si heshima kuendesha ufisadi. Waziri wawajibishe MD na Management yote ya EWURA, weka watu walio tayari kufanya kazi na Dkt. John Pombe Magufuli.