Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa fursa hii na nampongeza sana Mheshimiwa Waziri kwa wasilisho zuri asubuhi ya leo.

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli kwa kutimiza ndoto ya Hayati Mwalimu Nyerere ya kuanza kutekeleza mradi mkubwa wa kuzalisha umeme na Rufiji Hydro Power, maarufu Stiegler’s Gorge. Ushauri wangu, miundombinu wezeshi kuelekea eneo la mradi husuan barabara ya kutoka Kibiti kwenda Mloka iwekwe lami kurahisisha usafiri kati ya meneo hayo.

Mheshimiwa Spika, mradi wa REA katika Wilaya ya Mafia unaendelea vizuri na tunaishukuru sana Wizara na Serikali. Hata hivyo mradi wa kupeleka umeme wa jua (solar) katika visiwa vidogo vya Jibondo, Chole Jauni na Bwejuu ulikuwa uanze tangu Mwezi Septemba, 2018 lakini mpaka sasa hakuna dalili ya kuanza kwa mradi huo. Nichukue fursa hii kumuomba Mheshimiwa Waziri atuharakishie kuanza mradi huo na wananchi tulishaahidi na wamekuwa wakiulizia sana.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Mafia inapata umeme unaoalishwa kwa kutumia mafuta ya diesel na ni miongoni mwa wilaya chache ambazo bado hazijafungamanishwa na grid ya taifa. Natambua juhudi za Serikali katika kutuletea nishati mbadala kama umeme wa jua na umeme wa upepo. Ningependa kuishauri Serikali, kutokana kukua kwa shughuli za uzalishaji wa viwanda mahitaji ya umeme katika Kisiwa cha Mafia yanakaribia kufika megawatt 5. Namna bora kwa sasa ni kutuletea umeme kutoka nje ya Kisiwa cha Mafia kupitia uzamishaji wa nyaya chini ya bahari (sub-marine cables) katika umeme unazalishwa kwa vyanzo vya gesi kutoka Somanga Fungu.

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Ujazilizi (Densification) kwa Vijiji vya Wilaya ya Mafia. Nilete ombi rasmi kwa Vijiji vya Bweni, Kanga, Jimbo, Banja, Juju, Kiwenje, Balemi, Kifinge, Kunjwi, Kibada, Gonge, Ndagoni, Marimbani, Kiegeani, Chemchem, Mlongo, Mibulani na Dongo. Vijiji hivi vimepitiwa tu na mradi wa REA katika awamu hii.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Mafia imebahatika kuwa na kisiwa cha gesi eneo la Ndagoni kilichochimbwa na kampuni ya (M and P). Kwa bahati mbaya kwa awamu ya kwanza walikosa gesi baada ya kuwekeza fedha nyingi ilipokuja sheria mpya ya gesi (M and P) wanalazimika sasa kuomba upya leseni ya uchimbaji. Ushauri wangu kwa Serikali ni kuangalia namna ya kuleta amendments ya sheria kutoa mwanya kwa makampuni kama haya kuendelea na kazi za uchimbaji wa gesi katika Kisiwa cha Mafia.

Mheshimiwa Spika, (M and P) wamelazimika kutumia zaidi ya dola milioni moja kufukia kisima kule. La mwisho ni bei ya gesi asilia kwa viwanda kama Coca-Cola, Goodwill, Dangote n.k. ni kubwa, ipunguzwe.

Mheshimiwa Spika, nasukuru naunga mkono hoja.