Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekit, naomba kuchangia katika hoja hii kama ifuatavyo; kwanza naomba kuwashukuru kwa jitihada ya kuhakikisha umeme unaenea vijiji vyote vya Tanzania, hususan katika Mkoa wa Njombe.

Mheshimiwa Spika, kuna vijiji vya Matola, Mamanyolo, Kitulile, Luponde, Lugenge na vijiji vya Wilaya ya Ludewa Makete na Wanging’ombe bado havina umeme. Naomba Waziri atusaidie kuhakikisha vijiji vyote vvya Mkoa wa Njombe vinafikiwa na umeme.

Mheshimiwa Spika, pia hapa Dodoma kuna maeneo ambayo hayajafikiwa na umeme kama vile Kata ya Mtumba Mtaa wa Vikonje A karibu na majengo ya VIGUTA wananchi wanaomba umeme.

Mheshimiwa Spika, Kuhusu Gesi Asilia. Wananchi wengi wameshapata uelewa wa kutumia nishati ya gesi. Lakini tatizo ni kwamba gesi ni gharama. Naiomba sana Serikali ishushe bai ya gesi ili kupunguza uharibifu wa mazingira unaoendelea nchini.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.