Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Spika, Wizara hii ni muhimu kuelekea Serikali ya viwanda nchini, hivyo, kupitia hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imeishauri Serikali kwa sababu Wizara hii imeelemewa na inahitaji uzalishaji mkubwa na usambazaji wa kutosha kwa walipakodi, hivyo iko haja sekta ya uzalishaji na usambazaji vikajitegemea ili ifanye kazi kwa ufanisi na wananchi na wananchi wafikiwe na umeme kwa uhakika.

Mheshimiwa Spika, uunganishaji wa huduma za umeme; bado kuna tatizo gharama ziko juu, usumbufu kwa wananchi ambao tayari wameshaunganishwa na waliokamilisha mchakato lakini bado hawapati umeme, mijini na vijijini bado kuna tatizo. Tanzania ni nchi ya 83, kati ya 190 duniani kushindwa kuunganisha umeme kwa viwango, hivyo naishauri Serikali, iongeze juhudi katika kuwekeza kwenye ujenzi wa mabwawa na umeme wa upepo ili kupunguza pia gharama za umeme.

Mheshimiwa Spika, ukilinganisha gharama za umeme na Mataifa mengine Marekani 0.12, Ethiopia senti 2.4, Afrika Kusini 7.4, Misri 4.6, China na Korea senti 8.0 na Tanzania inalipa zaidi ya senti 10.7 dola kwa unit. Hiki ni kiasi kikubwa tofauti na nchi nyingine na hii inapelekea gharama za uzalishaji kuwa juu, production costs na hivyo kupelekea bidhaa kuwa juu nadhani Serikali ya Viwanda haitafikia malengo kama haitaweza kupunguza gharama hii.