Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

3

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, naipongeza Wizara ya Nishati kwa kazi kubwa wanayofanya hasa Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini (REA). Hata hivyo kasi ya utekelezaji wa mradi huu hasa kwenye Wilaya ya Karagwe na Jimbo la Korogwe Vijijini sio ya kuridhisha. Kwenye mradi huu kwenye Awamu III mzunguko wa kwanza Korogwe ilipangiwa vijiji 16 mpaka sasa umeme umewashwa kwenye vijiji saba tu.

Mheshimiwa Spika, tulileta maombi ya kupelekewa umeme kwenye vijiji 67 katika Mradi wa REA, awamu ya tatu, mzunguko wa kwanza. Ni vyema Wizara ituambie baada ya bajeti hii tutapata umeme kwenye vijiji hivyo vyote au hapana?

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na shida ya kuunganisha umeme kwa wakati, viko Vijiji vya Kulasi, Kibaoni na Mswaha Majengo vimesimikwa nguzo tangu mwaka 2018 mwezi Oktoba, lakini mpaka sasa umeme haujafika katika vijijji hivyo. Mkandarasi anasema tatizo ni tofauti ya transformer kati ya size inayotamkwa kwenye mkataba ambayo ni 33 kv na size ya line iliyopo ambayo ni 11 kv. Tofauti hii haijafanyiwa kazi muda mrefu na kusababisha malalamiko.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri alipofanya ziara Korogwe tarehe 19 Mei, 2019 alitoa maelekezo kuwa Kijiji cha Mahenge kipelekewe umeme. Umeme huo unatoka Kijiji cha Kerenge Kibaoni, Jimbo la Korogwe Vijijini lakini kuna vitongoji viwili vya Antakae na Mianzini vinapitiwa na umeme huo ukienda Mahenge. Naomba sana vijiji hivi visirukwe.