Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. PASCHAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia hotuba ya Wizara ya Nishati. Awali ya yote nitambue changamoto nyingi zinazoikabili Wizara hii ya Nishati japo Serikali kupitia Waziri na Naibu Waziri watazipunguza kama siyo kuzimaliza kabisa. Vivyo hivyo naamini document niliyompatia Waziri wa Nishati juzi tarehe 27 Mei, 2019 inayohusu tatizo la umeme Mtaa wa Shanko, Kata ya Vwawa itapatiwa ufumbuzi kwa kuwa eneo hili la Shanko limekuwa kama Kisiwa maana limezungukwa na umeme lakini lenyewe halina umeme.

Mheshimiwa Spika, eneo hili upande mmoja kuna kilomita mbili tu toka sehemu ya umeme na upande mwingine kilomita nne, hivyo Serikali ione namna ya kuwasaidia wananchi hawa.

Mheshimiwa Spika, mwisho japo siyo kwa umuhimu, naomba Serikali iwakumbuke wananchi wa Kata za Mara na Magamba Jimbo la Mbozi, kata hizi hazina umeme kabisa kijiji hata kimoja.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.