Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, kuhusu kutoa mwongozo rasmi kuwezesha TANESCO kuendeleza pale REA III inapoishia kabla ya kukabidhi mradi. Niwapongeze kwa kazi na hasa kwa kuanza kutuelewa watu wa Mafinga kwamba kutokana na uwepo wa viwanda vya mazao ya misitu, uhitaji wa umeme ni mkubwa, hivyo tunahitaji transfoma zenye capacity kubwa. Tayari tumepokea transoma mbili kati ya tano ambazo Mheshimiwa Waziri alituahidi wakati wa ziara ya Mheshimiwa Rais, hata hivyo, kuna jambo ambalo nashauri litolewe mwongozo.

Mheshimiwa Spika, kwa mfano sisi Mafinga baada ya wananchi kuona umeme unakuja, walijiandaa kuongeza shughuli za uzalishaji kwa kununua mashine kubwa za kuchana mbao, hata hivyo kutokana na scope kuwa ndogo, REA III haijawafikia wananchi wa aina hiyo ambao wapo tayari kujigharamia kwa kujiwekea nguzo kutoka pale ambapo scope ya REA III awamu ya kwanza imeisha. Hata hivyo, kwa kuwa utaratibu wa kiukandarasi na mikataba, TANESCO hawawezi kuendeleza pale mkandarasi alipoishia kwa kuwa mradi bado haujakabidhiwa rasmi kwa TANESCO na hasa ukizingatia kuwa kuna miezi kumi na miwili ya matazamanio.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu hiyo, naomba Wizara itoe mwongozo rasmi wa kuruhusu hasa maeneo mahususi ambayo wananchi wapo tayari kujigharamia kwa nguzo kama ilivyo katika baadhi ya maeneo ya Mafinga. Naamini kwamba nimeeleweka, maana kuna maelezo lakini hayajanyooka kwa maana kwamba kanuni na taratibu zinataka TANESCO aendelee baada ya kukabidhiwa mradi na ndiyo maana nashauri kuwa patolewe mwongozo rasmi kuhusu suala hilo.

Mheshimiwa Spika, Mafinga kuwa na wilaya ya ki- TANESCO; suala hili nimelileta mara kadhaa, hata hivyo sijui kama naeleweka. Mufindi ni wilaya ambayo ina viwanda vingi vya chai, karatasi na viwanda vya mazao ya misitu. Hata makusanyo (revenue) inayokusanya ni makubwa kushinda hata baadhi ya mikoa. Hivyo, hili ni eneo ambalo lina potential kubwa sana. Hata hivyo, shughuli za viwandani zinapoteza wastani wa 30% ya muda wa kufanya kazi kutokana na ama kukatika umeme au hitilafu hasa nyakati za mvua. Kwa kuwa tunategemea connection iliyopo Mgololo, ikitokea fault yoyote, umeme unakatwa ili kurekebisha hizo faults.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo ombi letu, tuwe na TANESCO Mafinga (kama ilivyo Dar ambapo kuna wilaya za TANESCO nje ya wilaya za kiutawala mfano Tabata, Mikocheni na kadhalika). Tunaomba hivi kutokana na hali halisi ya uhitaji na pia kusogeza huduma karibu kwa wateja, lakini pia kwa kuwa eneo hili lina potential kubwa maana yake ni kuwa tutaongeza revenue ya TANESCO.

Mheshimiwa Spika, pia hii itawezesha TANESCO Mafinga kuhudumia viwanda vya mazao ya misitu na wakazi wa maeneo jirani wakati TANESCO Mufindi itahudumia viwanda vya chai na wakazi wa Mufindi. Mimi siyo mtaalam lakini naamini nimeeleweka, na rejea zangu za maandishi kwa barua zipo katika ofisi za TANESCO na REA.

Mheshimiwa Spika, densification hasa Kitelewasi, Shule ya Sekondari Mnyigumba na kadhalika. baadhi ya vijiji kama vile Kitelewasi ambapo kuna Shule ya Sekondari Mnyigumba walipata umeme REA II ambapo scope haikufika maeneo yote ikiwemo Shule ya Sekondari Mnyigumba ambapo tulihitajika kulipia milioni 78. Suala hili nimeshalifikisha kwa maandishi na barua Wizarani na REA, hivyo naomba densification iweze kujumuisha maeneo ya Kitelewasi na Kijiji cha Kikombo.

Mheshimiwa Spika, vijiji mbadala na upatikanaji wa materials kwa ajili ya TANESCO; kuna maeneo ambayo tumewasilisha REA kupitia TANESCO kwa ajili ya reviewed scope ambapo kuna eneo Ifingo, Kinyanambo Sekondari, Banda Beach, Lumwago na Isalavanu Primary School. Pia kuna maeneo ambako line kubwa ilipaswa kujengwa na mkandarasi lakini tayari maeneo hayo yalishajengwa line kubwa na hivyo tunaomba gharama zilizokuwa zijenge line kubwa, basi mkandarasi aelekezwe kupeleka umeme maeneo ya nyongeza ya Lumwago, Zanzibar na Banda Beach. Haya yote hasa kuhusu vijiji mbadala yapo tayari REA.

Mheshimiwa Spika, upatikanaji wa materials; kama nilivyosema awali, yapo maeneo TANESCO wanaendelea kwa mfano Mwongozo, Ifungo na Makamadoresi ambako kuna shule ya watoto wadogo inayoendeshwa na Masista. Tunaomba TANESCO wapelekewe materials kwa wakati.