Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Spika, nichukue fursa hii kwanza kuunga mkono hoja iliyopo mezani. Pili, kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na uongozi mzima wa Wizara kwa kazi na jitihada ambazo wamefanya hususani katika kuwapelekea Watanzania umeme.

Mheshimiwa Spika, binafsi nitakuwa mnyimi wa fadhila kama sitomshukuru Waziri na Naibu wake kwa ziara zao walizofanya Jimboni kwangu, hakika zimezaa matunda.

Mheshimiwa Spika, baada ya pongezi hizo, naomba sasa nijielekeze juu ya vijiji vyangu ambavyo havijapata umeme. Kilindi ina vijiji 102 na vitongoji 615, lakini ni vijiji 50 ambavyo mpaka sasa vitakuwa au vinatarajia kuwa na umeme, vijiji 52 havina umeme kabisa. Niombe sana tena vijiji 52 vilivyobaki vipatiwe umeme na naamini kabisa vijiji hivi navyo vitapata katika awamu ya tatu ya REA III.

Mheshimiwa Spika, kwa hali ya jiografia ya wilaya yangu ilivyo ina changamoto nyingi sana, hii ni pamoja na kukatika kwa umeme mara kwa mara na hii inasababishwa na idadi ya watumiaji imeongezeka na chanzo pekee cha umeme ni kutoka Mkata, Wilaya ya Handeni. Kwa kiasi kikubwa umeme umekuwa ukikatika mara kwa mara ni kuwa kero kubwa kwa watumiaji, lakini pia hii imekuwa sehemu ya Ofisi ya TANESCO Kilindi kuendesha ofisi kwa gharama kubwa sana.

Mheshimiwa Spika, natambua jitihada za Wizara za kufanya interconnection network ya kutoka Mbigili, Wilaya ya Kiteto hadi Kufungu kilomita 55; mradi huu ni muhimu sana kwani utakuwa ni suluhu ya kupata umeme wa uhakika. Pia ningeomba kama tungepata network interconnection kutoka Kikunde hadi Kukivu kilomita 41 ambayo itasaidia Vijiji vya Ludeva, Mafalila, Tunguli, Mtoro na Kitingi vitafaidika na umeme.

Mheshimiwa Spika, vijiji tajwa hapo juu vipo mbali na Makao Makuu ya Wilaya, mfano Kijiji cha Kikunde, Kata ya Kikunde umeme umetokea Wilaya ya Mvomero, Morogoro. Niiombe sana Serikali iitazame Kilindi kwa Kijiji cha Tatu.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.