Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Spika, awali nawapongeza Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Watumishi wote wa Wizara ya Nishati kwa hotuba nzuri na kwa kazi nzuri wanayoendelea kuifanya.

Mheshimiwa Spika, naipongeza Serikali kwa Mradi wa Stiegler’s kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini kwetu, huu ni mradi wa ukombozi. Tunahitaji umeme mwingi sana wa megawatts 2,100 za Stiegler’s zitatupaisha katika huduma za maji, afya, elimu, viwanda, reli (SGR) na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, kwa miradi ya REA ahadi zitekelezwe. Kijiji cha Kondo, Kata ya Zinga kilikuwa katika orodha ya REA III, lakini mpaka mwisho wa mradi (Juni, 2016) mradi haukutekelezwa na katika REA IIIA Kondo haimo, lakini Mheshimiwa Waziri aliahidi miradi ambayo haikutekelezwa katika REA II itapewa kipaumbele katika REA III. Naomba Mheshimiwa Waziri aelekeze Mradi wa Kijiji cha Kondo utekelezwe haraka wananchi hao wamesubiri muda mrefu sana, tangu 2013.

Mheshimiwa Spika, kwa ufanisi wa miradi ya REA nashauri REA izingatie mapendekezo ya Wabunge yaliyowasilishwa kwa utaratibu uliowekwa yaani kupitia TANESCO (W) na TANESCO (M). Katika Jimbo la Bagamoyo, vitongoji saba (Kata ya Denda) vyenye umeme viliorodheshwa katika REA IIIA wala havikupendekezwa na Mbunge wala TANESCO (W) wala TANESCO (M). Wataalam wa REA wazingatie mawasiliano ya Wabunge ikiwezekana mapendekezo ya Wabunge ndiyo yafanyiwe kazi ilimradi yamepitia utaratibu uliowekwa.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.