Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja hii. Hongera nyingi kwa Waziri, Naibu Waziri na timu yote ya Wataalam wa Wizara. Mambo ya msingi:-

Mheshimiwa Spika, kwanza, Wizara ifanye fast track ya miradi ya kuunga Mkoa wa Kigoma kwenye gridi ya Taifa:-

(a) Tabora-Kigoma na Nyakanazi-Kigoma. Miradi hii ni muhimu sana, vinginevyo Mkoa wa Kigoma utabaki nyuma kama ilivyo sasa, lazima tuonyeshe tofauti.

(b) Mradi wa Malagarasi Hydro Power MW 45.4; mradi huu ni muhimu sana kwa nchi na Mkoa wa Kigoma, kupata MW 45.4 ku-feed kwenye grid ni kitu kizuri na muhimu sana. Ushauri wangu kwa Wizara ni kwamba wapeni kipaumbele mradi huu, tumeusubiri sana. Hoja ya upungufu wa fedha haina nguvu ya kimkakati, ikibidi tukope fedha tujenge mradi huu, ni muhimu sana.

(c) Malipo ya fidia; Malagarasi na Kidahwe itakapojengwa sub-station ya grid. Walipeni fedha hizi haraka ili kazi ianze kwa jinsi ratiba ya utekelezaji ilivyopangwa. Miradi hii kwa Kigoma si tu ni muhimu, hii ndiyo roho ya mkoa wetu.

Mheshimiwa Spika, pili, REA lll Kigoma, Kasulu, Buhigwe, Uvinza na Mradi huu ulizinduliwa kule Rusesa, Kasulu DC mwaka jana 2018. Speed ya mradi huu ni ndogo sana, mkandarasi aongeze nguvu. Tangu uzinduzi ule, maeneo mengi hata vifaa havijapelekwa yaani nguzo, nyaya na kadhalika. Tafadhali kasi iongezeke.

Mheshimiwa Spika, tatu, mradi wa ujazilizaji wa maeneo (densification round two). Halmashauri ya Mji wa Kasulu-TC, kata nyingi zaidi ya tisa zilipata umeme wa REA ll, tatizo/shida ni kwamba, maeneo karibu yote umeme umefika sehemu moja tu. Mfano umeme umefika sokoni, umeme umefika Ofisi ya Mtendaji na kadhalika. Umeme haujafika kwenye mitaa, vitongoji walipo wananchi wetu wengi. Nishauri strongly, Mkoa wa Kigoma sasa uingizwe kwenye huu mradi wa ujazilizi hasa katika Mji wetu wa Kasulu. Ikiwa ni heshima kwa Serikali mikoa iliyopata shida ya kuanza REA lll basi ipate nafuu ya kupata mradi huu.

Mheshimiwa Spika, Kijiji/Kata ya Mrufiti, kata hii ilisahaulika wakati wa survey, nilimshauri Regional Manager TANESCO Kigoma akiingize kijiji hiki ambacho pia ni kata ili iende sambamba na maeneo ambayo yamefanyiwa survey ya Kigondo, Muhunga, Ruhita, Ngumbigwa na sasa Mrufiti. Hii ni muhimu sana ili wananchi hawa wasionekane wametengwa kwa sasa. Maeneo yote ya jirani yamefanyiwa survey hiyo, hii ya kusema Mrufiti isubiri phase two ya survey iondoke. Wananchi hawa wanataka umeme leo.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.