Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Spika, nawapongeza viongozi kwa kazi nzuri wanazofanya. Mheshimiwa Waziri Dkt. Medrad Kalemani na Naibu Waziri Mheshimiwa Mgalu, hongereni sana. Mchango wangu utajikita katika maeneo matatu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, vijiji vilivyo kwenye line kubwa Mtwara-Nanyamba Newala, vijiji takribani nane vipo chini ya line hii. Nimpongeze Waziri kwa maagizo yake ambayo aliyatoa hivi karibuni akiwa Mtwara kuwa vijiji hivyo vipewe umeme. Nashauri TANESCO Mtwara wawezeshwe ili waweze kutekeleza maelekezo hayo.

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya Majengo; kituo hiki kipo Kata ya Njengwa na hakuna umeme. Namshukuru Waziri kwa kuelekeza TANESCO Mtwara kuwa waanze mpango wa kuleta umeme katika kituo hiki. Nashauri msisitizo utolewe ili kiweze kupata umeme ili kiweze kutoa huduma zilizokusudiwa.

Mheshimiwa Spika, mradi wa kusambaza gesi majumbani; mradi huu ni muhimu na naomba fedha zitengwe za kutosha ili idadi ya nyumba/kaya zitakazopewa gesi ziongezeke katka Miji ya Mtwara, Lindi na Dar es Salaam. Pia na maeneo mengine na wilaya zake na si Makao Makuu ya Mikoa tu.

Mheshimiwa Spika, kukosekana kwa umeme katika baadhi ya Mitaa-Nanyamba Mjini; naomba Mitaa ya Madina, Namkuku na Kilimanjaro iliyopo Nanyamba Mjini iwekewe umeme.