Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. ENG. GERSON H. LWENGE: Mheshimiwa Spika, pongezi kwa Mheshimiwa Waziri na Naibu na Watendaji. Pongezi kwa kuzalisha umeme na kuwa na ziada ya MW 300 na hivyo kutokuwepo mgao wa umeme. Rufiji Hydro Power MW 2,115. Kuongezeka kwa kasi ya kuwaeleza umeme vjijini na kufikia vijiji 7,127 kati ya vijiji 12,268 na kufikia Juni 2020 vitafikia 10,268. Pongezi kwa uamuzi wa kutoza 27,000 kuunganisha umeme vijijini japo lina changamoto na linakwamisha wananchi hasa inapotakiwa kununua nguzo, maelekezo shilingi 27,000 ndani ya mita 30.

Mheshimiwa Spika, REA III, mzunguko wa kwanza, lengo vijiji 10,278 by June 2020, mzunguko wa pili lengo vijiji 1,990 kuanza Julai 2020.

Mheshimiwa Spika, Wanging’ombe vijiji 54 hivi sasa havina umeme kabisa, mzunguko wa kwanza vijiji na vitongoji 48, vijiji 38 na vitongoji 10 pogram todate vijiji vinne na vitongoji vitano. Mkataba unaisha Disemba, 2019. Swali, atakamilisha vijiji 39 ndani ya miezi sita? Mkataba umeonesha anasambaza line kubwa kilomita 95 wakati uhalisia kufikia vijiji 48 ni kilomita 150 mpaka leo addendum ya scope na muda haijasainiwa.

Mheshimiwa Spika, mkandarasi Mufindi power JV Hegy Engineering, utendaji wa kazi hauridhishi kabisa, bado maeneo ya vijiji 27 vilivyo kwenye mkataba aidha hajapeleka nguzo kubwa au hajatandaza wire au hajaanza hata kupeleka nguzo ndogo. Mkandarasi huyu hata hivyo vijiji vinne na vitongoji vitano inachukua zaidi ya miezi mitatu kuwasha umeme toka wateja wailipe TANESCO kwa madai kuwa mita zilifungwa bila kusajiliwa.

Mheshimiwa Spika, Meneja wa TANESCO Wilaya hana gari la kufuatilia utekelezaji wa mradi huu.

Mheshimiwa Spika, kuunganisha umeme kwa wananchi 27,000 iwe ni ndani ya mradi au vinginevyo. Maelekezo ni kwamba, Sh.27,000 ni ndani ya mita 30; nguzo moja Sh.391,000, nguzo mbili Sh.450,000, halafu nguzo inakuwa mali ya TANESCO utakuta watakaofuata wanalipa Sh.27,000 tu. TANESCO wapewe bajeti ya kuweka nguzo.

Mheshimiwa Spika, hivi vijiji vimepewa scope ya wastani wa kilomita mbili, kwa hiyo eneo kubwa la kijiji na vitongoji havijapewa umeme. Sasa maeneo haya yaliyosalia pamoja na vijiji ambavyo havijafikiwa vimewekwa kwenye awamu ipi? Kwani kwenye hotuba page 61 Waziri ameongelea kuhusu idadi ya vijiji ambavyo havitafikiwa ifikapo Juni 2020, hajasema chochote kuhusu vijiji vilivyopewa scope kidogo, page 65 haielezei scope jazilizi na hakuna bajeti.

Mheshimiwa Spika, uendelevu wa mradi huu kabambe wa REA; mwaka jana nilishauri sambamba na kuwekeza fedha nyingi kwenye ujenzi wa mradi Serikali iwekeze fedha ya kutosha za matengenezo ili kuiwezesha TANESCO kuhimili mahitaji ya matengenezo, sijaona mpango huo kwenye bajeti hii. Mfano 90% Road Fund ni matengenezo; 7% Road Fund ni mwendeleo ujenzi mpya; 2% Road Fund ni utawala. Wilaya ya Wanging’ombe REA II transfoma 30. REA III transfoma tisa zimeungua wako gizani. Seven transformers are replaced but two not yet for more than six months.

Mheshimiwa Spika, mikataba; yapo majukumu (obligations) za mwajiri client na yapo majukumu (obligations) za mkandarasi. Mkandarasi lazima alipwe kwa wakati (30 days) baada ya kuidhinisha hati ya madai. Mkandarasi asipofikisha lengo la utekelezaji zipo hatua za kuchukua. Kila mwezi kuna Progress Site Meeting, hizi lazima zisimamiwe vizuri na Consultant na client. Tusisubiri mwisho wa muda ndio tuchukue hatua au zinaanza kuzuka hoja eti mkandarasi hana uwezo, swali alipataje kazi? Tathmini ya uwezo kikazi na kifedha ilifanyike (due diligence)?

Mheshimiwa Spika, orodha ya vijiji vilivyomo REA III round I navyo ni Ihanja, Lusisi, Mungate, Itambo, Udonja, Ujange, Kasagala, Lugoda, Ikwega, Matowo, Itowo, Ilulu, Gonelamefuta, Masage, Mapogoro, Ukomola, Saja, Igomba, Isimike, Mtewele, Ujindile, Uhambule, Msimbazi, Igelango, Mng’elenge, Ufwala, Katenge, Mbembe, Itandula, Mpululu, Igelehedza, Igula, Mayale, Ing’enyango, Ivigo, Luduga sekondari.

Mheshimiwa Spika, vijiji visivyokuwepo kwenye REA III round 1. Idunda, Masaulwa, Ikwavila, Uhenga, Mbembe, Ikulimambo, Idenyimembe, Igenge, Idindilimunyo, Iyayi, Igando, Hanjawanu, Mpanga, Malangali, Wangamiko, Litundu.