Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Spika, umeme unaleta maendeleo kwa wananchi na kuongeza uzalishaji katika viwanda na itapelekea kuinua uchumi wa nchi yetu. Naiomba Serikali kupeleka umeme wa REA katika Jimbo la Mufindi Kusini. Vijiji vingi ambavyo havijapata umeme kabisa katika Jimbo la Mufindi Kusini ni kama ifuatavyo:-

(1) Kata ya Idunda, Vijiji vya Idumulavanu, Ikangamwani na Mkangwe;

(2) Kata ya Itandula, Vijiji vya Ihawaga, Nyigo, Ipilimo na Ikiliminzowo;

(3) Kata ya Mtambula, Vijiji vya Ipilimo, Iyegela, Nyakipambo, Mtambula na Mzumbiji;

(4) Kata ya Kasanga, Vijiji vya Ihomasa, Kilolo na Udumka;

(5) Kata ya Kiyowela, Vijiji vya Magunguli, Kiyowela na Isaula;

(6) Kata ya Idete, Vijiji vya Itika, Holo na Idete:

(7) Kata ya Maduma, Vijiji vya Wangamaganga, Maduma na Ihanganatwa;

(8) Kata ya Nyololo, Vijiji vya Njonjo, Lwingulo na Nyololo Shuleni;

(9) Kata ya Mninga, Vijiji vya Mkalala, Ikwega, Itulituli na Kitilu;

(10) Kata ya Luhunga, kijiji cha Ihefu;

(11) Kata ya Malangali, Vijiji vya Isimikinyi, Kingege na Itengule;

(12) Kata ya Ihowanza, Vijiji vya Idope, Ipilimo, Igenge na Kiponda.

Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali kupeleka umeme katika kata na vijiji vyote ambavyo nimevitaja, pia kuna vitongoji zaidi ya 30 havijapata umeme, zahanati, vituo vya afya, shule za msingi na shule za sekondari bado hazijapata umeme wa REA.

Mheshimiwa Spika, kata na vijiji hivyo survey tayari na baadhi ya kata na vijiji ambavyo nimevitaja nguzo tayari bado waya na sehemu nyingi nguzo na waya tayari bado kuwasha. Naiomba sana Serikali kukamilisha mradi huu wa umeme wa REA ili wananchi wa Jimbo la Mufindi Kusini kufanya shughuli zao na kuinua uchumi wao.

Mheshimiwa Spika, ahsante na naunga mkono hoja.