Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia hoja iliyoko mezani. Kwanza niishukuru Serikali, nimshukuru Mheshimiwa Waziri, Naibu, Katibu Mkuu na Idara zote zilizopo chini ya Wizara.

Mheshimiwa Spika, kwanza nipende kutoa pongezi kwa Taasisi ya REA, kwa kweli kazi inayofanywa ni kazi nzuri na tunaiona. Nakini nipende kusema kwamba kwa Ludewa bado mkandarasi hafanyi vizuri sana kwa sababu mpaka sasa ni kijiji kimoja tu ndicho kimewashwa. Kwa hiyo ninaamini kwamba kwa jitihada za Mheshimiwa Waziri na Mtendaji na Mkuu wa REA kadiri tunavyokuwa tunazidi kuwasiliana ninaamini kwamba sasa hivi mkandarasi atajiweka sawa na kuweza kwenda vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nianze kuongelewa vyanzo vya nishati, hasa umeme. Tumeona kuna umeme wa maji, kuna umeme wa gesi, kuna umeme wa makaa ya mawe, upepo na jotoardhi; nianze na maji. Tunavyo vyanzo vingi sana vya maji na hasa hata kwetu kule Ludewa tuna mito mingi sana ambayo inamwaga maji ziwa nyasa na inaweza ikawa ni miongoni mwa vyanzo vizuri vya umeme.

Mheshimiwa Spika, Kwa hiyo ningeomba sasa Wizara ijipange na iweke master plan ya maeneo yote ambayo yanaweza kuwa ndiyo chanzo kikubwa cha umeme wa maji ambao ndio unaonekana ni rahisi. Kwa hiyo kuna haja sasa Serikali ikaweka mpango mkubwa na tuweze kuona ni namna gani tunaweza tuka-meet zile megawatt 10,000 ambazo Serikali imezipania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Spika, tunao umeme wa makaa ya mawe na hata nchi nyingi sasa hivi, including Marekani inaanza kutumia umeme wa makaa ya mawe. Tunayo makaa ya mawe pale Mchuchuma ambayo yanaweza yakatoa megawatts 600. Kwa hiyo, naamini kwamba Serikali ikijipanga vizuri, ikachukua na kuanzisha utaratibu mzuri wa kuweza ku- tap yale makaa ya mawe pale bado Serikali na nchi itaweza kufaidika kwa kiasi kikubwa na tukawa na umeme wa kutosheleza kwa sababu tayari tumejipanga kwamba Serikali na nchi imejipanga katika mfumo wa viwanda na viwanda vinahitaji umeme. Kwa hiyo kuna haja sasa makaa ya mawe kule Mchuchuma yakawa ni moja kati ya resourceful ya kuweza kufikia hizi megawati 10,000.

Mheshimiwa Spika, lengo letu kufika 2025 ni kuwa na megawati 10,000 sasa labda pengine nijaribu kuangalia mpango ukoje wa Serikali ili kuweza kufikia hizo megawati 10,000 tunazoziendea, kwa sababu naamini kwamba tuna ile mipango ya kufikia ule muda wenyewe na kuna ile mipango ya mwaka mmoja mmoja na kuna ile mipango ya kati. Sasa Serikali ije na majibu tuone kwamba mpaka sasa kwa mwaka huu ni…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)