Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuchangia kwenye hotuba hii ya Wizara ya Nishati. Kwanza kabisa nichukue fursa hii niungane na Waheshimiwa Wabunge kuwapongeza Mheshimiwa Waziri wa Nishati Mheshimiwa Kalemani na Naibu wake Mheshimiwa Subira Mgalu, kwa sababu hawa ni Mawaziri ambao wanasikiliza Wabunge na wanachukua hatua kwa vitendo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitazungumzia bomba la mafuta ambalo linalotoka Uganda mpaka Tanga. Katika bomba lote hili la mafuta jimboni kwangu Kata ya Igusule, Kijiji cha Sojo ndipo itajengwa kambi na kituo kikubwa cha kuyafunika mabomba ili yasipate kutu na kuweza kuzuia joto mabomba yote ya njia nzima coating itafanyika pale Igusule ambapo ndio kijiji kwangu.

Mheshimiwa Spika, shughuli ya kujenga hiki kituo pale kijijini itaingiza bilioni 600. Ni shughuli kubwa sana bilioni 600 zitaingia pale. Sasa hoja yangu hapa ni local content, ni namna gani wananchi, Watanzania wa Kijiji cha Igusule, Jimbo la Bukene na Wilaya ya Nzega na Watanzania wote watanufaika na huu uwekezaji wa hizi bilioni 600.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu kwa Wizara tuna Sheria ya Mafuta ya mwaka 2015 ambayo ina kipengele cha ushirikishwaji wa wananchi, ningeomba Wizara ijipange kutumia sheria hii ili kwa makusudi kuwa na mpango wa makusudi wa kusaidia Watanzania hasa wa Jimbo la Bukene pale Igusule kuhakikisha kwamba wananufaika na hizi bilioni 600. Hivyo, lazima kuwa na mpango wa makusudi, kwa hivyo watu wa maeneo yale lazima tujue kazi zitafanyika pale, kazi za ujuzi, kazi za ujuzi wa kawaida, vibarua, huduma mbalimbali ambazo zitatolewa pale na Serikali imejipangaje ili kuwasaidia kwa makusudi watu wa maeneo yale waweze kufaidika na uwekezaji wa bilioni 600.

Mheshimiwa Spika, hili jambo tukiliacha hivi hivi, Watanzania wananchi wa Nzega, wananchi wa Jimbo la Bukene tukiacha hivi hivi bila hatua za makusudi, tunaweza tukajikuta bilioni 600 zimewekezwa pale mradi ukaisha, lakini ukipima manufaa ya wananchi wa pale utakuta kwamba hawajanufaika chochote. Tunachohitaji watu wa pale ni kwamba, hali za maisha za wananchi wa maeneo yale ambapo bilioni 600 zitawekezwa Igusule, Jimbo zima la Bukene na Wilaya nzima ya Nzega hali zao za maisha baada ya uwekezaji wa bilioni 600 ni lazima zibadilike zi-reflect kweli kuna bilioni 600 ziliingia, otherwise kutakuwa hakuna manufaa yoyote ya bilioni 600. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo ushauri wangu kwa Wizara hapa ni kwamba, lazima kuwe na mpango wa makusudi, hapa na-underline neno makusudi; mpango wa makusudi, ukiacha kama ilivyo wananchi kwa kweli bila kusaidiwa, bila kuwa na mpango maalum, tutashangaa bilioni 600 zimewekezwa, lakini wanaweza wakaja watu ambao sio Watanzania, wajanja wengine ndio wakanufaika zao. Kwa hiyo lazima tulindwe, tuwe protected ili tuweze kunufaika na hizi.

Mheshimiwa Spika, hili la Miradi ya REA limeongelewa na Wabunge wengi, kwa hiyo ushauri wangu ni kwamba natambua jitihada za Mheshimiwa Waziri Dkt. Kalemani na Naibu wake katika kuwasukuma wakandarasi ili waweze kutimiza majukumu yao lakini pamoja na jitihada hizi bado wakandarasi wanasuasua katika maeneo mengi kama ambavyo Waheshimiwa Wabunge wamesema.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu kwamba mwishoni wakati Mheshimiwa Waziri ana-wind-up atueleze ili tujue tatizo ni wakandarasi au tatizo ni Wizara…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana.

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja na ahsante sana. (Makofi)