Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii nami niungane na wenzangu wote kwamba nami natambua kazi inayofanywa na Waziri, Naibu Waziri na watendaji wote wa Nishati.

Mheshimiwa Spika, napenda nijielekeze sasa kwenye Wilaya yangu halafu baadaye nitaongea habari ya Stiegler’s Gorge pamoja na fidia kuhusu gridi ya Taifa. Wilaya Hanang ina vijiji 96 na ni moja ya Wilaya mbili, Mbulu na Hanang ndio tulipewa vijiji vichache sana mwanzoni, baadaye nikaongea na Waziri akaongezea vijiji, lakini kuna vijiji 30 ndio vipo kwenye mpango wa kuletewa umeme, lakini spidi ni ndogo na bado 40 hawajui ni lini kwa sababu kuna ahadi ya Serikali lini vijiji vyote vitapata, nafikiri atafanya kila linalowezekana na bado ahadi yake ya tarehe 2 kwenda kwenda Hanang pamoja name ipo pale ili tukaangalie matatizo ya Vijiji vya Hanang. Naomba sana spidi ya contractor iangaliwe.

Mheshimiwa Spika, la pili ni kuhusu Gridi ya Taifa, kuna maeneo ambayo gridi ya Taifa imepita na wameahidiwa wapate fidia na wanalia kila siku hasa vijiji, hivyo naomba sana fidia ile iweze kupatikana.

Mheshimiwa Spika, sasa naomba nijielekeze kwenye Stiegler’s Gorge mimi ni moja kati ya watu mbao tunafurahi sana mradi wa huu unatekelezwa katika nchi hii. Na sisi wote humu ndani tunajua chanzo cha maji kwa umeme ndio chanzo ambacho kina gharama ndogo na hatimaye bei ya umeme itakuwa ndogo na ndio itakayochochea viwanda nchi hii. Kwa hiyo namshukuru sana Rais na ninashukuru Serikali nzima kujielekeza kwenye Stiegler’s Gorge jambo ambalo kwa kweli litawafanya wananchi wa Tanzania wapate umeme ambao sio ghali.

Mheshimiwa Spika, nataka niwambie wale ambao hawaelewi vyanzo vyote ni vyetu vya gesi vya jua vya maji na hata ile nuclear bado ni chanzo chetu tunacho, ni lazima tuchague vyanzo vile ambavyo tukianza navyo vitatuletea manufaa makubwa na Stiegler’s Gorge ni mahali ambapo tutapata kweli gharama ndogo.

Mheshimiwa Spika, nakumbuka wakati NGO’s zikipiga kelele kwa ajili ya Stiegler’s Gorge isitumiwe kama chanzo cha umeme walikuwa wanaongelea chura, jamani utalinganisha chura na wananchi? Haiwezekani! Namshukuru sana Rais huyu kwa kuwa imara na kuwa na ujasiri wa kukataa mambo ambayo hayana sababu na wengine wote humu ambao wanawaunga mkono wale watu kwa sababu zingine mbalimbali, naomba tuwe pamoja kwa hili kwa sababu ni manufaa ya Taifa hili la Tanzania, tumpe moyo Rais wetu na Waziri wetu ili waweze kukazania na hata kama hela itachukuliwa mahali pengine kwa manufaa ya sekta zote tusiwe na malalamiko ili tuwe tunapitisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi, watu wa Hanang wanaomba Mradi wa REA, wanufaike nao kama wilaya zingine zinavyonufaika na wale ambao hawapata fidia waweze kupata fidia.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono kwa moyo wangu wote bajeti hii ya Waziri Kalemani na Serikali hii. (Makofi)