Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Katani Ahmadi Katani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tandahimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. KATANI A. KATANI: Mheshimiwa Spika, kwanza nichukue fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu, lakini nikushukuru wewe pia kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, nami niungane na wenzangu kumpongeza Waziri na Naibu wake kwa kazi kubwa wanayoifanya. Lakini nina mambo kadhaa ambayo ningependa nipate ufafanuzi.

Mheshimiwa Spika, jambo la kwanza, sisi Mtwara pale tuna mitambo ya kuzalisha umeme, tunayo mitambo 11. Na Mheshimiwa Waziri unajua kila mtambo mmoja unazalisha megawati mbili kwa maana ya mitambo yetu 11 inazalisha megawati 22, japo miwili ni mibovu, na ninajua una taarifa hiyo.

Mheshimiwa Spika, lakini kwenye matumizi ya Mkoa wa Mtwara na Lindi kwa maelezo ya nyie wataalam wa umeme mnasema tunatumia megawatts 15 na tunakuwa na ziada ya megawats tatu, mara nyingi huwa napata shida mnaposema tunaziada ya megawatt hizo tatu kwasababu kama leo Tandahimba yenye vijiji 156 ina vijiji takriban 88 havina umeme lakini ukichukulia hesabu ya mkoa mzima wa Mtwara una vijiji vingi havina umeme kuliko vyenye umeme. Sasa sijui hii extra inaonekana kwamba inapelea, inapelea namna gani wakati watu kule hawapati umeme mtatusaidia kitaalamu zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini nirudi kwenye suala la mradi huu wa REA Mheshimiwa Waziri nashukuru sana tumekuwa tukiwasiliana mara kwa mara juu ya mkandarasi ambaye tunaye Mtwara, kwenye Jimbo langu nina vijiji 30 ambao vilitakiwa viwe na umeme na mkataba baina ya Serikali na yule Mkandarasi unaishia tarehe 30 Juni ya kesho kutwa lakini mpaka sasa ninapozungumza na wewe vijiji vitatu ndiyo wamewasha umeme sina hakika hizi siku zilizobaki anaweza kuwasha umeme kwa vijiji 27 ambavyo vimesalia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini niliwahi kukwambia kwa Jiografia ya kwetu kwa Jimbo langu la Tandahimba maeneo makubwa yenye watu wengi nikakwambia juzi nilikutumia na meseji Kata kama Mdimba ina wapiga kura tu elfu nane na kitu. Maana yake hiyo sehemu ina watu zaidi ya 12,000 au 13,000 na Kata nyingi za Tandahimba zina uwingi wa watu ukienda Tandahimba kwa uzalishaji wa korosho wa miaka mitatu, nyumba nyingi zimeshafanya wiring zinasubiri mapokeo ya umeme ukienda nyumba nyingi zimefanya wiring. Leo watu wanapata shida ya umeme ambao tuliamini kabisa kwa sisi watu wa Mtwara ambao gesi ambao tunasema asilimia 50 ya umeme tunaotumia ndiyo unatokana na gesi, lakini Mkoa wa Mtwara ndo unalalamika hauna umeme. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niliwahi kwenda kwa Mheshimiwa Simbachawene nikapata maajabu makubwa vijiji vyake vyote vinawaka umeme. Lakini Mtwara ambako gesi inatoka leo tunakaa kulalamika umeme, umeme, umeme sasa hili Mheshimiwa Waziri niombe mnafanya kazi kubwa sana lakini kwa watu wale wa Mtwara ambao wameathirika kwa kiasi kikubwa na mradi ule tukazungumza habari ya mabomba hayo wale hawana umeme wapelekeeni umeme basi iwe kifuta jasho chetu tumepata umeme na wale wanauwezo wa kulipa hiyo 27,000 hata mngesema walipe 50,000 wanauwezo wa kulipa lakini umeme haujawafikia watu wa Mtwara.

Mheshimiwa Spika, nimuombe sana kwenye jambo hili tunapoenda kwenye REA hii basi uingize vijiji vile vilivyobaki tuone suala la umeme kwa namna mlivyoandika hiyo 2021 watu wawe wamepata umeme. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini mwanzo mlizungumza suala la viwanda ambavyo mama Ghasia amegusia suala la kiwanda cha Mbolea Msanga Mkuu, lakini mlizungumza suala la kiwanda cha Mbolea Kilwa Masoko kwenye kitabu chote cha Wizara sijaona hilo jambo sasa wakati una-windup utatuambia kwamba haya mambo ya viwanda hivi vya mbolea Kilwa Masoko, Mtwara kama vimepotea tujue vimepotea na kama vipo tujue vipo kwenye hatua gani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nizungumzie suala la LNG ambayo wenzangu wamepongeza. Nipongeze lakini napata mashaka makubwa sana jambo hili limekuwepo tangu tunazungumzia suala lenyewe la gesi 2010 likazungumzwa suala la LNG Lindi, na tukaamini tutakuwa miongoni mwa maeneo ambayo uchumi wake ungepanda kwa kasi kusini ni pamoja na kama mngekweli mngejenga hii LNG. Leo mmehuisha mazungumzo kama mnavyosema tuone sasa haya mazungumzo mnayoyasema…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)