Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ili niweze kuchangia katika Wizara hii ya Nishati. Kwanza kabisa nimpongeze Waziri Mheshimiwa Dkt. Kalemani, Naibu wake, dada yangu Mheshimiwa Subira Mgalu kwa kazi anayoifanya, lakini pamoja na timu yao yote, wanafanya kazi kubwa sana kwa kweli mwenye macho haambiwi tazama. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitajikita kwenye mada moja tu, hususan katika kutaja vijiji vyangu vyote ambavyo havina umeme, pamoja na shule, pamoja na zahanati. Ni imani yangu kubwa kwamba Mheshimiwa Kalemani alifika Lushoto na akatoa maelekezo kwa Wakandarasi, lakini Mkandarasi yule, bado hajatekeleza ahadi ya Waziri mpaka leo. Sasa kwa kuwa leo timu nzima leo ipo hapa basi nami nianze Kijiji kimoja baada ya kingine ili wataalam wake wakusaidie kusukuma mambo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na vijiji ambavyo havina kabisa umeme katika Jimbo la Lushoto ambavyo ni Vijiji vya kwanza Miegeo, Handei, Ngulwi, Kwemashai, Gare, Yamba, Kongei, Masange, Makanka, Milungui, Kireti, Kigumbe, Bombo Kamgobore, Kilole, Mazumbai, Ntambwe, Mavului, Mazashai, Mdando, Kweulasi, Bombo, Kwetango, Mbwaya, Kigulunde na Kwai. Hivyo ni vijiji kabisa ambavyo havina umeme kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vinavyofuata ambavyo ni vya kujaziliza ni Vijiji vya Chumbageni, Ngulwi, Kizara, Yoghoi, Magamba, Kilangwi, Kwemashai, Boheloi, Migambo, Kwefingo, Kwemakame, Malibwi, Mbwei, Mshangai, Makole, Mlola, Ungo na Mhezi.

Mheshimia Naibu Spika, nimeamua kuyataja maeneo yangu kwa sababu Mheshimiwa Waziri alikuwa kila siku ananiambia nimletee orodha, kwa hiyo leo nimeamua kutaja orodha hii moja kwa moja kwa sababu wataalam wake wote wapo, basi waichukue na waendelee kumsukuma sana yule Mkandarasi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niendelee na sekondari ambazo hazina umeme ni Sekondari za Balozi Mshangama, Masange, Gare, Mkuzi, Kwai, Kwekanga, Mariam Mshangama, Makole, Mdando, Kweulasi na Mazashai. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, hapo hapo bila kupumzika niendelee na Vituo vya Afya na Zahanati. Kituo cha Afya Gare, Zahanati ya Makanka, Kituo cha Afya Ngwelo ambayo ni Kigulunde, Zahanati za Miegeo, Mavului, Mazumbai, Mbelei, Kweulasi na Mdando. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimeyafanya hayo, maana nimechoka kuandika na hansard nayo ichukue ili Waziri akihitaji basi atachukua tu kiurahisi. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimeyataja hayo maeneo yote hayo lakini kila eneo nililolitaja hapo lina shule, lina Msikiti na Zahanati…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)