Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa nafasi hii; na kama ilivyoada ningependa kutoka sakafu ya moyo wangu niwapongeze sana Mheshimiwa Waziri na Naibu wake na Wizara kwa ujumla kwa kufanya kazi nzuri sana ya kusambaza umeme katika nchi yetu. Kazi mnayofanya inaonekana nasi ni wajibu tuwapongeze.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kazi nzuri na kubwa kila siku lazima kunakuwa na mashimo na madoa ambayo lazima yanyooshwe. Ningependa niende kwenye jimbo langu; niseme mpaka mwisho wa mwaka uliopita wananchi wa vijjini kule Mwanga walikuwa wakinunua umeme wa shilingi 5,000 wanapata unit 43 za umeme. Mwisho wa mwaka jana ukawa ndio mwisho wa furaha. Tangu mwaka huu uanze shilingi elfu 5 ile ile wananunua unit 13 umeme umepanda kwa asilimia 330.

Mheshimiwa Naibu Spika, niliuliza juu jambo hili wakati wa briefing na Mheshimiwa Naibu Waziri akinipa jibu sijui niliite jibu la namna gani; akasema watu wa mwaka wote waliopewa umeme wameanzisha viwanda kule nyumbani. Kwa hiyo kwa sababu wameanzisha viwanda wanapata umeme kwa bei ya watu wenye viwanda. Sasa nimetafuta vile viwanda kule Mwanga sijaviona. Mheshimiwa Waziri ninakuomba kesho ukifanya majumuisho hili jambo la kuwabagua watu wa Mwanga kama wamekuwa watu wa viwanda wote liachwe. Watu wa Mwanga wapate umeme wapate umeme kama wananchi wa Tanzania wanaoishi vijiji.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, muda ni mdogo, lakini ningependa nizungumzie kidogo nizungumzie juu ya REA III. Nimshukuru Mheshimiwa Waziri na Naibu wake walitembelea kwenye jimbo langu, na kazi kwa kweli kwa span imefanya; lakini yapo maeneo ambayo span inayotolewa ya kuwafungia watu umeme inatuletea matatizo kule vijiji. Kwa mfano kwenye Kijiji changu cha Kigonigoni wananchi wanaotaka umeme wapo 380. Watu waliopo kwenye scope ya kupewa umeme ni watu 38, na kijiji chote watu wanakaa mahali pamoja si kijiji ambacho kimesambaa kwenye eneo kubwa; ukiongeza nguzo hamsini unawapa wote umeme. Sasa ninaelewa mambo ya span na mambo ya menejimenti, lakini na ninyi muelewe siasa pia na mtupunguzie malalamiko ya wananchi. Kama kinachotakiwa ni nguzo 50 leteni nguzo ... (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)