Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi hii; nami nitakuwa na mambo matatu tu. Nitazungumzia grid ya Taifa kwa mikoa ya Kigoma na Katavi, nitanzungumizia mradi wa Stiegler’s Gorge maarufu mradi wa umeme Rufiji halafu nitanzungumzia mradi wa densification, ujazilizaji baada ya ufanisi katika mikoa hii minane ambayo imekamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza Mheshimiwa Waziri nikupe hongera sana kwa kazi, wewe na Naibu wako mnafanyakazi nzuri mnazunguka nchi yetu vizuri sana na mnafanya kazi nzuri sana. Kwa hiyo wewe na timu yako TANESCO, REA, TPDC mnafanya kazi nzuri sana hongereni sana sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na mradi huu wa grid ya taifa kwa Mkoa ya Kigoma na Mikoa ya Katavi. Katika nchi yetu ni mikoa miwili ambayo haijaunganishwa kwenye grid ya taifa; lakini nashukuru kupitia hotuba yako ya leo umezungumzia juhudi kubwa iliyopo ya kuunganisha Mikoa ya Kigoma na Katavi kwenye grid ya taifa. Ombi langu la msisitizo wangu kwako na ushauri kwa Serikali ni mikoa miwili tu imebaki kuunganishwa kwenye grid ya taifa.

T A A R I F A

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Nsanzugwanko kuna taarifa.

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika nampa taarifa mzungumzaji anasema mikoa miwili sijui Rukwa ameisahauje? Si mkoa? Ni Wilaya ya Rukwa?

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Nsanzugwanko unaipokea taarifa hiyo.

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Naibu Spika, sina hakika na Rukwa kwa sababu Rukwa wanapata umeme kutoka Zambia sasa sina hakika sana, nami napenda nizungumze vitu nina hakika navyo. Ambayo nina hakika ni Mkoa wa Kigoma na Mkoa wa Katavi, wenzetu wa Rukwa wanapata kidogo kutoka Zambia.

Mheshimiwa Naibu Spika, na hoja yangu ni dogo tu, kwa kuwa kuna shughuli mnafanya ya kuunganisha mikoa hii miwili, Mheshimiwa Waziri na timu yako niwaombe muipe priority mikoa hii. Bila kunganisha kwenye grid ya taifa ni impossible, haiwezekani, haiwezeikani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama tunavyofahamu kwamba umeme ni roho ya uchumi, umeme ni maisha; kwa hiyo nikuombe Mheshimiwa Waziri mikoa hii miwili sasa kwa mujibu wa hotuba yako hapa ipeni priority, ipeni kipaumbele iweze kuunganisha na gridi ya taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya yangu ya pili ni Rufiji Stiegler’s Gorge. Mradi huu wa Stiegler’s Gorge ni muhimu sana kwa taifa, ni mradi ambao wala hatupaswi kujadiliana; huwezi kuwa na nchi ambayo haina umeme

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nimebahatika kwenda kutembelea bwawa la Aswan Dam kule Misri. Roho na ujeuri wa nchi ya Misri ni Bwawa la Aswan, wanapata umeme mwingi sana. Kwa hiyo Mheshimiwa Waziri tunakuunga mkono kwa nguvu zetu zote, Watanzania tupo nyuma yako, tupate umeme mwingi na wa kutosha. Kwa hiyo mradi muhimu sana, mradi wa kiuchumi, Mheshimiwa Waziri songambele taifa lipo nyuma yenu.

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja yangu ya tatu ni huu mradi wa kujaziliza maeneo ambayo yana umeme. Mheshimiwa Waziri umefika Kigoma mara tatu sasa, tulizindua REA three kule Lusesa; tunashukuru sana kwa hotuba yako nzuri uliyoitoa. Baadaye ulikuja mpaka Luhita kule kwangu, umefanya kazi kubwa, hongera sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kuna huu mradi wa densification program au mradi wa kujaziliza maeneo yaliyobaki. Nimesoma kwenye hotuba yako Mheshimiwa Waziri ukurasa wa 65 unasema kuna mikoa ile minane ambayo imakamilika; sasa nilikuwa naomba hii mikoa miwili ambayo tumechelewa kupata umeme wa REA II na REA III bado inasuasua. Nikuombe sana katika hii awamu inayokuja round two basi Mkoa wa Kigoma na Mkoa wa Katavi; nasisitiza mikoa hii miwili kwa sababu ni special kwa sababu ni mikoa ambayo haiunganishwa na grid ya taifa. Nikuombe katika hii pragramu ya densification mkoa wa Kigoma na mkoa wa katavi uipe kipaumbele.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho; lipo jambo mahususi kabisa. Umeme unaohudumia Wilaya mpya ya Buhigwe unatoka mjini Kasulu. Sasa vipo vijiji na maeneo ambayo watu wanatazama umeme na umepita kwenye maeneo yao. Nikuombe Mheshimiwa Waziri jambo hili nimeshakueleza, nikuombe ulipe kibaumbele. Yale maeneo ambayo umeme umepita katika vijiji vyao wasije wakahujumu miundombinu yetu, nakuomba sana maeneo hayo yaweze kupata umeme.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo naunga mkono hoja hii muhimu sana, nasema ahsante sana.