Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili nami niweze kuchangia. Kwanza nianze kwa kuwapongeza Wizara, Mheshimiwa Waziri, Naibu wake na timu nzima ya Wizara yake kwa uwasilishaji wa bajeti katika kipindi hiki kinachokuja cha 2019/ 2020, lakini kwa namna ambavyo wamejipanga katika kuhakikisha kwamba wanaendelea kuleta mapinduzi makubwa ya umeme katika nchi yetu na kuhakikisha kwamba tunajipanga kwa ajili ya uwekezaji na kukuza uchumi lakini kukuza ajira katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niendelee kuipongeza Serikali kwasababu iko miradi mbalimbali ambayo inaendelea kutekelezwa, lakini mingine iko katika mpango wa utekelezaji na hii yote ina dhamira njema ya kuzalisha umeme katika nchi yetu kwa sababu bado tunahitaji matumizi makubwa ya umeme katika nchi yetu katika kuhakikisha kwamba tunaendelea kujipanga vizuri katika kuleta mapinduzi haya ambayo tunayategemea.

Mheshimiwa Naibu Spika, niendelee kusema kwamba katika mradi huu wa REA ambao Waheshimiwa Wabunge wengi wameusemea. Nimebahatika kupita katika maeneo mbalimbali tukiwa katika ziara ya Kamati katika kukagua miradi mbalimbali ambayo inaendelea na tumeendelea kuwasha umeme katika vijiji vingi nchini Tanzania. Kwa hiyo bado hali si mbaya sana ya umeme katika maeneo ya vijiji umeme unaendelea kuwekwa, lakini tunaamini kwamba vijiji vinaendelea kukua siku hadi siku, miji pia inatanuka au inaendelea kukua, kwa hiyo mahitaji ya umeme bado ni makubwa. Kwa hiyo niishauri tu Serikali kwamba katika eneo la REA basi ni vyema tukaongeza wakandarasi ili kazi zikaenda kwa spidi ambayo tunaitarajia kwa sababu kila mmoja wetu hapa anahitaji katika eneo lake basi vijiji vyote viwe vimefikiwa umeme kwa wakati mmoja jambo si rahisi sana kwetu, lakini tukijipanga vizuri basi angalau mwaka 2020 basi maeneo mengi yatakuwa yameweza kufikiwa na huu umeme wa REA.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri na timu yake; walikuja kupitia shirika la TPDC katika Mkoa wetu wa Lindi na walikuja kutuelimisha na kutoa elimu mbalimbali. Tumejionea mambo mbalimbali kupitia mkutano ambao tumeufanya katika Mkoa wetu wa Lindi. Kaimu Mkuu wa Mkoa alimshauri Waziri kwamba makandarasi yule anaonekana hayuko tayari kufanya kazi katika Mkoa wa Lindi. Sasa tuliomba tubadilishiwe mkandarasi yule aweze kuwekwa mkandarasi mwingine ili mambo yaweze kwenda vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie suala mradi wa LNG, kama alivyotangulia kusema mdogo wangu Mheshimiwa Bobali pale, ni mradi mkubwa ambao tunautegemea katika mkoa wetu wa Lindi tuweze kuupokea ingawa tumeupokea tangu mwaka 2014.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kila mwaka tunatenga fedha za kuwalipa fidia wapisha mradi wa LNG katika eneo la Likong’o. Miaka minne mfululizo bajeti inakuwa inatengwa lakini fedha haitoki kwa ajili kuwawezesha ndugu zetu ambao wanapisha mradi katika eneo hili la likong’o. Sasa nilikuwa naiomba sana Serikali…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)