Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

Hon. Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Spika, napenda kuunga mkono hoja na kuwapongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watumishi wote kwa kazi nzuri zinazoonekana kufanyika.

Mheshimiwa Spika, napenda kujua hatma ya maeneo ya Jimbo langu ambalo kuna dhahabu. Eneo hilo lipo Sakale, Amani na Mheshimiwa Waziri amefika eneo hilo na kuzungumza na wananchi. Nakushukuru ulituma wataalam wa sekta zote ambazo walifika eneo hilo, lakini bado hawajatoa taarifa yao. Namhakikishia Mheshimiwa Waziri pamoja na madini hayo kuwa karibu na chanzo cha maji ya Mto Zigi, lakini naamini tunaweza kukubaliana njia bora na ya kisasa kuweza kuchimba utajiri huo kitaalam. Naomba alipe umuhimu suala hili ambalo linanipa tabu sana Jimboni.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.