Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Salum Mwinyi Rehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nami nilitaka nitoe shukrani kwa uwasilishaji wa hotuba hii ya Waziri kuhusu bajeti ya elimu. Nilikuwa na mambo ambayo yananisikitisha na hasa kuhusiana na mfumo mzima wa elimu unavyokwenda hapa Tanzania. Kwa kiufupi kusema ukweli, hakuna consistency ambayo tunaiona inatolewa kwa elimu yetu katika level zote. Tuchukulie mfano kule Zanzibar, safari hii wamesema wameanza kufanya mitihani ya Darasa la Sita. Ukitoka Darasa la Sita unaaza Form One.
Mheshimiwa Mwenyekiti, watoto hawa wanaoanza shule miaka minne, miaka mitano anaanza Darasa la Kwanza, akifika Darasa la Sita, ana umri gani? Halafu arukishwe aende Form One. Mtu huyo huyo anatakiwa afanye Common Exam Form Four, ambayo inasimamiwa na NECTA. Huku Tanzania Bara Darasa la Saba, lakini Form Four wanafanya Common Exam. Sasa hizi elimu tunaiga mifumo ya nje ambayo kwa kweli haijafanyiwa uchunguzi na utafiti wa kutosha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimefanya utafiti katika Jimbo langu la Uzini na nilikuwa naandaa strategic plan. Preliminary survey niliyokuwa nimeifanya matatizo niliyoyakuta ndani ya lile Jimbo, kuna tofauti kubwa baina ya shule na shule ndani ya Jimbo, achilia mbali ndani ya Wilaya. Tofauti nyingine iliyokuwepo, ni baina ya shule za private na shule za Serikali, there is no common syllabus. Kila mmoja anaangalia mazingira ya uboreshaji wa elimu kwa eneo lake.
Sasa kwenye Serikali unajiuliza, tofauti ya syllabus hii ya Serikali inatofautiana baina ya shule moja na shule nyingine, lakini kubwa linatokana na kwamba hakuna monitoring, ufuatiliaji haupo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wakaguzi ndio wanaoweza kupita katika zile shule wakaweza kuhakikisha kwamba syllabus inayofundishwa pale ni sahihi. Shule zetu nyingi nyingine zinatumia mitaala inayotoka Cambridge, nyingine zinatumia mitaala ya Kenya nyingine zinatumia mitaala waliyotengeneza wenyewe kulingana na mazingira yao; ndiyo maana unakuta level ya upasishaji inakuwa tofauti baina ya eneo moja na lingine. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri kama tuna Common Exam, lazima tuwe na mtaala mmoja na flow iwe inaeleweka kutoka chini kuja juu. Flow yetu iliyokuwepo ndiyo kitu kinachotutesa. Kila mmoja anakwenda njia yake. Nchi hii hatutafika kwa kila mmoja kwenda vile anavyoona yeye. Leo ukienda St. Mary‟s na shule nyingine za mission zina miongozo na mitaala yao na kiwango chao cha elimu kinachotolewa ni tofauti kabisa na shule nyingine za private, lakini halikadhalika shule nyingine hizi za vipaji maalum zina miongozo yake na mitaala yake mbalimbali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri kwamba tukae pamoja, kama ni NECTA na wadau wake wengine ili kuweza kutoa common syllabus itakayoweza kufuatwa, lakini vilevile ile consistency ya madarasa tukubaliane, kwa sababu wale Wazanzibari wanasema wao wakiona flow imekwenda vizuri mwakani nao Tanzania Bara inataka kuanza mwisho Darasa la Sita, haieleweki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapoamua jambo, tujiandae kwanza, tufikiri hawa wanafunzi kweli tunataka kuwapa kitu gani na kwa level gani? Mtoto akimaliza Shule ya Msingi, Darasa la Sita, huyo anamaliza Form Four bado mdogo sana na uwezo wa kukabili mtihani wa Form Four unakuwa haupo. Sasa nashauri kwamba mkutane viongozi wa elimu wa sehemu hizi mbili ili kuwe na mustakabali mzuri wa kuweza kuendesha hizi shughuli na mambo yaweze kwenda vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo linakwaza kwenye elimu ni suala zima la ukosefu wa Walimu husika kwa masomo husika. Shule zetu nyingi Walimu wamekuwa wanabambikiziwa masomo ambayo hawana ujuzi nayo. Mwalimu amesomea arts kwa vile hakuna Mwalimu wa science, anapewa science anaambiwa bwana utaziba kiraka.
Vilevile Mwalimu amesoma science sekondari, pengine Form Two au Form Three, lakini leo ndiyo unamweka Mwalimu huyo aweze kufanya practicals za chemistry na physics kwa wananfunzi wa Form Four. Sasa kwa kufanya hivi, tunaziba viraka. Hii siyo elimu ambayo tunategemea kwamba itaweza kuwasaidia Watanzania. Kuwepo na utaratibu maalumu wa kuajiriwa Walimu wapelekwe katika maeneo maalum ili kuwe na uwiano wa utoaji wa elimu. Vinginevyo bado tutaendelea hapa kuhangaika na kutengeneza bajeti na kushauri lakini hakuna kinachoendelea. Elimu inaporomoka kwa mfumo huo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine kinachotofautiana, shule nyingi zimejenga maabara, lakini tatizo la vifaa vya maabara limekuwa sugu na haviko katika shule chungu nzima. Na leo tuna lengo la kuhakikisha kwamba tunainua elimu ya sayansi katika nchi hii. Watu wale waliokuwa wamejenga maabara pengine inawezekana kwa shinikizo, kwamba lazima iwepo maabara pale, hapana walimu, vifaa vile hata kama wanavipeleka walimu waliokuwepo hawana uwezo wa kufanya zile practical. Kwa hiyo, mtu anakuwa na majengo na vifaa ambavyo havitumiki. Nakuomba Mheshimiwa Waziri hili nalo ukae na timu yako …