Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

Hon. Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

MHE. ZAINAB M. AMIR: Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri kwa kazi kubwa wanayoifanya katika Wizara hii kwa kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali ifuatavyo:-

Kwanza, fedha zinazotengwa katika bajeti zitolewe kwa wakati ili Wizara iweze kutekeleza majukumu yake kwa wakati.

Pili, itoe elimu ya kutosha hususani kwa wachimbaji wadogo wadogo jinsi ya utunzaji wa mazingira ukizingatia wakati wachimbaji madini huacha mashimo makubwa ambayo huharibu mazingira yetu. Elimu itolewe ili baada ya kuchimba wayafukie mashimo hayo.

Tatu, iwapatie wachimbaji wadogo wadogo zana/ vifaa vya kufanyia shughuli zao za uchimbaji ili waweze kupata madini kwa urahisi pia kuweza kupata mapato kwa Taifa.

Nne, iandae vifaa vya uokoaji vya kutosha katika migodi yetu ili pindi zikitokea ajali za kufukiwa wachimbaji ndani ya migodi iwe rahisi kuwaokoa.

Tano, ili kukuza soko la ndani la madini kwa kuvutia wawekezaji, Serikali iendelee kuwatafutia wachimbaji wadogo masoko ya uhakika ili kuuza madini yao ndani ya nchi na kuepusha utoroshwaji wa madini nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, mwisho, namwomba Mungu ampe afya njema na umri mrefu Mheshimiwa Waziri wa Madini pamoja na Naibu Waziri ili kuweza kutekeleza majukumu yao ya kila siku.