Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

Hon. Sonia Jumaa Magogo

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

MHE. SONIA J. MAGOGO: Mheshimiwa Spika, nianze kwa kuipongeza Wizara kwa kazi nzuri na jitihada kubwa tunazoziona katika kuiendeleza hii tasnia. Pamoja na pongezi hizi niombe Wizara izingatie sana changamoto zinazowakabili hasa wachimbaji wadogo. Mojawapo ikiwa ni ufahamu mdogo wa Sera ya Madini inayopelekea kushindwa kukuza shughuli zao na wengi kuishia kupata hasara.

Mheshimiwa Spika, lingine ni suala la mitaji; wachimbaji hawa wadogo hasa wanawake wapewe mitaji hata mikopo toka katika mabenki kwa kutumia leseni zao na hata madini ambayo wanayo.

Mheshimiwa Spika, kuna changamoto nyingine ya masoko ya uhakika kwa madini yanyopatikana wengi hawajui exactly masoko watapata wapi na hata bei zinazoendana na ile wanachokipata hivyo kupelekea kuuza bidhaa zao chini ya bei. Wachimbaji hawa wangepewa elimu juu ya madini mbalimbali na hata dalili za kuwa sehemu fulani kuna madini ya aina fulani ili kupunguza tatizo la kuhama hama linalochangia kuleta hasara.

Mheshimiwa Spika, pia manyanyaso dhidi ya wachimbaji hasa wadogo wadogo yadhibitiwe ili kuwajengea mazingira mazuri ya kazi zao.

Mheshimiwa Spika, ahsante.