Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Spika, masuala nyeti ya uwazi kwenye tasnia ya uziduaji yanayohitaji majibu ya Serikali; mchango wangu wa hotuba hii ya Wizara ya Madini mimi ni mdau wa madini natoka katika maeneo yenye machimbo, hivyo mchango wangu unajikita katika hatua kadhaa zinazochukuliwa katika utekelezaji wa Sheria ya Uwazi katika Tasnia ya Uziduaji ya mwaka 2015. Uwazi unasaidia kuzuia makandokando ya rushwa, matumizi mabaya ya madaraka, utakatishaji wa fedha haramu na utoroshwaji haramu wa fedha kutoka kwenye Sekta ya Madini, Mafuta na Gesi. Hivyo, nitazungumzia mambo manne muhimu kuhusu uwazi katika tasnia ya uziduaji (madini, mafuta na gesi asilia).

Mheshimiwa Spika, nitaeleza athari za uwazi kuhusu kampuni 23 za uziduaji kutoorodheshwa katika Soko la Hisa Dar-es-Salaam. Katika mchango wangu nitaomba Serikali ituambie hatua za utekelezaji wa kanuni za mwaka 2019 zilizotungwa ili kuweka wazi majina ya watu watatu ambao ni wanufaika wa umiliki wa makampuni ya uziduaji.

Mheshimiwa Spika, nitawataja wanasiasa na wenye maslahi yenye kutia shaka katika kampuni za uziduaji (political exposed personalities). Sheria hizi za makampuni zinaiweka Tanzania katika nchi zilizo hatarini kutumiwa na wahuni kuficha mali za wizi kwenye tasnia ya madini, mafuta na gesi.

Mheshimiwa Spika, Kampuni 23 za Uziduaji Kutoorodheshwa katika Soko la Hisa Dar-es-Salaam. Kati ya kampuni 54 za tasnia ya uziduaji ni kampuni nne tu ndio zilizoorodheshwa katika soko la hisa la Dar-es-Salaam (Dar e s Salaam Stock Exchange). Establishment Maurel et Prom Swala Oil & Gas (Tanzania) Public Limited Company. The Tanzania Cement Company Limited na TOL Gases Limited.

Mheshimiwa Spika, kampuni 23 za uziduaji kutoorodheshwa soko la hisa. Kampuni 23 kati ya 54 ni kampuni zinazomilikiwa na umma huku kampuni zao kuu zikiwa zimesajiliwa nchi za Canada, Kenya, Norway, South Africa na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, ukiangalia leo kwenye soko la hisa (Dar es Salaam) ni kampuni 28 za sekta mbalimbali zinazouza hisa zake katika soko hilo huku Sekta ya Madini, Mafuta na Gesi zikiwa kampuni nne pekee. Endapo kampuni hizi za gesi na madini zikiorodheshwa katika Soko la Hisa Dar es Salaam fursa ya uwazi itafunguliwa kutokana na kanuni za uendeshaji wa soko hilo zilivyo, wamiliki halisi wa kampuni watakuwa wazi hivyo kuondoa dhana ya rushwa, matumizi mabaya ya madaraka na utakatishaji wa fedha haramu.

Mheshimiwa Spika, naomba Waziri akija hapa kuhitimisha hoja yake aseme ni kwa nini wasilete marekebisho ya Sheria ya Uwazi katika Tasnia ya Uziduaji ili kiwepo kipengele kinachowalazimisha kampuni zote za uziduaji kuorodheshwa katika Soko la Hisa Dar-es-Salaam. Waziri Biteko alitunga sheria Februari, 2019 kuhusu uwazi na uwajibikaji kwenye tasnia ya uziduaji, hivyo zielekezwe.

Mheshimiwa Spika, tungeweza kuwabaini hawa wanasiasa na watumishi wenye maslahi katika madini, lakini tunashindwa kubaini kwa sababu Sheria ya Maadili inazuia kuweka wazi. Hapa hakuna uwazi. Majibu nahitaji?

Mheshimiwa Spika, Waziri akija hapa kuhitimisha aseme ni kwa nini Serikali isilete sheria ya makampuni au sheria ya uwazi katika tasnia ya uziduaji, ili kuzuia uhuni.