Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

Hon. Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia Wizara hii kwenye maeneo makuu mawili; mosi, ulipaji wa fidia kwa wakati na kwa wananchi wote waliopo kwenye maeneo yaliyochukuliwana na Mgodi wa Acacia North Mara. Maana kuna baadhi ya nyumba hazijafanyiwa tathmini kabisa na yapo maeneo ya operesheni za mgodi. Hivyo, Waziri anapokuja kuhitimisha atueleze hatua zilizochukuliwa kwa hizi familia na lini wanalipwa sanjari na wengine wanaosubiri malipo tangu mwaka 2009.

Mheshimiwa Spika, baadhi ya hizo familia zilizopatwa na madhara kutokana na operesheni kama vile vumbi, mishtuko wakati wa blasting, kubomoka kwa nyumba; mfano ni Simon Mikulabe, Max, Ibrahim, Max, Prisca Chacha, Chacha Ihande, Abel Max, Mwita Tall, Amos Atendo, Mwita Nyamhanga, Chacha Tall John, Mwikabe Bina, Amos Atendo Nyankobe, Mhere Wagi na wengine.

Mheshimiwa Spika, kuna baadhi waliachwa kwenye zoezi la uthamini No. 20 ndani ya buffer zone kwa sababu mbalimbali kama vile kutokuwepo wakati wa tathmini (safarini), wengine walikuwa gerezani. Raia hawa wameshafika mgodini na kuongea na uongozi wa mgodi juu ya uthamini. Hata hivyo mgodi wanasema Serikali inasitisha uthamini hadi itakapotoa kibali tena. Tunaomba kauli ya Serikali juu ya hatua ya hizi familia zilizopo ndani ya buffer zone.

Mheshimiwa Spika, vilevile ninataka kujua, katika ile faini waliyotozwa Acacia dhidi ya uchafuzi wa mazingira Wananyamongo wanafaidika vipi kwa kupewa fidia hasa wale walioathirika na uchafuzi wa mazingira?

Mheshimiwa Spika, pili ni kuhusu Mgodi wa Kabanga ulioko katika Mji wa Tarime ambao wachimbaji wadogowadogo wamekuwa wakipata matatizo mengi kwa kunyanyaswa na watu wenye fedha (kama Mzungu) na hata wengine kupelekwa gerezani wakati wanachimba kwenye maeneo yao halali.

Mheshimiwa Spika, hili jambo nilishalifikisha Wizarani kipindi Mheshimiwa Kairuki akiwa Waziri na hata kwa Kamishna wa Madini wa Kanda yetu na mkoani wanajua. Hili eneo la Kabanga inasemekana leseni ni ya Barrick, kwa muda mrefu tumeomba iweze kufutwa na leseni zipewe kwa wachimbaji wadogowadogo ili wafanye uchimbaji wao kwa uhuru zaidi bila kubugudhiwa. Pale kuna wajane wananyanyasika sana. Pale kuna mkandarasi tu ndiye ana leseni na hiyo ya Barrick. Wanakabanga tunapenda kujua kama leseni ya Barrick imeshafutwa ama bado na kama imefutwa kwa nini leseni hawajagaiwa wale wachimbaji wadogo wadogo.

Mheshimiwa Spika, pili, mkishawapa leseni watakuwa wmaepata sifa ya kupewa ruzuku ili wajiendeleze kwenye Sekta ya Uchimbaji na kufaidika na rasilimali zilizopo kwenye maeneo yetu.

Mheshimiwa Spika, kwa hayo machache, naomba kuwasilisha.