Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

Hon. Jumanne Kibera Kishimba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kahama Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

MHE. JUMANNE K. KISHIMBA: Mheshimiwa Spika, yeah, ahsante sana; na mimi niungane na Wabunge wenzangu kuwapongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri na Watendaji wote Idara ya Madini kwa kazi nzuri wanayofanya.

Mheshimiwa Spika, mimi ninayo shida kubwa sana kwenye Mgodi wangu wa Buzwagi. Mgodi huu unaenda kufungwa au kufukiwa; mgodi huu juzi kwenye ziara ya Makamu wa Rais Mheshimiwa Naibu Waziri Nyongo alikuwepo na Mawaziri wengine; Meneja wa mgodi alituhalifu kwamba mgodi ule bado una balance ya dhahabu ounce audhi milioni moja, ni sawa sawa na kilo 31 za dhahabu. Anachodai Meneja wa mgodi ni kwamba gharama zao za uzalishaji ni kubwa.

Mheshimiwa Spika, kilo 31 ni sawa sawa na dola bilioni 1,200,000 ambazo ni sawa na trilioni 28. Kinachonishangaza hapa; ni kweli tukubali kwenda kufukia mgodi wenye dhahabu ya trilioni 28 ilhali sisi tunauwezo wa kufunga mto Rufiji tukapata umeme?

Mheshimiwa Spika, lawama lazima tuitupe tu kwa wataalamu ukweli ni wavivu kwa kufikiri, hauwezi ukaletewa ripoti na mtu mmoja mwenye mgodi akafukia mgodi wako wenye thamani ya trilioni 28 na wewe unashida ya kujenga Standard Gouge wewe uko tayari kuziba mto Rufiji, haiwezekani, ni kitu ambacho kinauzunisha sana. Serikali kwenye Sheria yetu mpya ana asilima 16 mle ndani ina maana na Serikali atapoteza na kodi tutapoteza. Lakini alichosema Meneja wa mgodi ni kwamba gharama zao ni kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa mimi niombe kwa Mheshimiwa Waziri au wewe utusaidie. Iundwe tume ndogo iende ikaangalie gharama za uzalishaji za mgodi huo; zile ambazo zinaweza kuondolewa ziondolewe. Lakini Serikali upande wake pia ifikirie; maana TANESCO anapata bilioni mbili kwa mwezi, TRA anapata na yeye zaidi bilioni 20 Idara ya Maji tunapata zaidi ya bilioni nne. Hawa kama wanaweza na wao kupunguza tariffs zao wapunguze maana kama mgodi utafungwa hata hizi tariffs zao hazitafanya kazi popote. Ikiwezekana wapunguze ili tuunusuru mgodi huu.

Mheshimiwa Waziri tumekuwa tukiongea mara kwa mara lakini bado mimi nawasiwasi kwamba wataalam wetu ni wavivu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili ni suala zima la madini. Utajiri wa Warabu ni mafuta, na Warabu wamepata utajiri wa mafuta pale bei ya mafuta inapopanda. Sisi tunayo dhahabu, wahasibu wetu wanachanganya kati ya hesabu ya kiwanda na hesabu mining. Dhahabu haipandi kwa ajili ya gharama ya uzalishaji, dhahabu inapanda kwa hali inayoendelea duniani. Kama kuna hofu au tatizo lolote dhahabu itapanda.

Mheshimiwa Spika, sasa nachojaribu kujiuliza hapa; na nafikiri Mheshimiwa Waziri itabidi hapa nishike shilingi ili tupate ufumbuzi. Bei ya dhahabu mwaka 2008 ilikuwa gram moja ni dola 40, ambapo ni kama ounce moja dola 800; leo ni dola 60; lakini gharama za uzalishaji hazikupanda, maana raw material ya dhahabu ni mawe ambayo ni asilimia 70, kilichoongezeka hapa hakikuongezeka kwa sababu ya gharama ya uzalishaji, kimeongezeka kwa sababu ya demand duniani tofauti na kiwanda. Serikali ya Tanzania kama wahasibu au wataalam wetu watakubali, tunakuwa na utajiri mkubwa sana pale bei ya dhahabu inapopanda; ile pesa si pesa ya mweye mgodi wala mwenye mgodi hawezi kuidai, kwa sababu hata dhahabu isipopanda yeye anaendelea na uzalishaji na faida anapata. Warabu wametajirika ni pale bei ya mafuta inapopanda duniani, ile tofauti inatakiwa kuwa yote ni mali ya Serikali siyo mali ya mwenye mgodi . Maana yake hiki ni reserve ya ile nchi ndiyo faida yake iko hapo; wataalam naona bado linawapa shida sana suala hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa ajili ya muda naomba niungane kwenye suala moja na Mheshimiwa Heche. Mheshimiwa Heche amesema, ni kweli ile migodi haijawahi kutulipa service levy yetu mpaka sasa hivi. Service levy hiyo anayoisema inahitaji ufafanuzi kidogo; ni kwamba hizi mining zote zilizoko Tanzania zina bima tatu, zina bima ndani ya dhahabu inapokaa, zina bima ya mgodi mzima, zina bima zinapotaka kwenda kukopa benki maana yake zote zimekopa benki lazima ziweke bima; kwa hiyo zina bima tatu. Bima hizi ni zimelipiwa Ulaya kweli, lakini kwenye tariff ya TRA wame-deduct kama cost. Kwa hiyo zile pesa tunatakiwa sisi tulipwe service levy yetu ambayo ni zero point three.

Mheshimiwa Spika, Kwa hiyo hii pesa siyo ya mgodi ni ya yule mtu wa insuarance ambaye yupo; ni watu wa mgodi tu kutuambia kwamba ni huyu hapa na invoice tumpelekee, si mali ya mgodi hata siku moja na hawa watu wa insurance hawajawahi kujulishwa mimi ninavyojua; na watakataa kwa sababu hawajawahi kulipa kitu chochote wana benefit wao. Ingetusaidia sana, kama alivyosema Mheshimiwa Heche na Mheshimiwa Musukuma kwamba ni vizuri watusaidie.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naunga mkono hoja. (Makofi)