Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Dr. Immaculate Sware Semesi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI: Mheshimiwa Naibu Spika, sababu kuu zinazosababisha uharibifu katika misitu/ uvunaji wa kupitiliza na usio endelevuni;

Mheshimiwa Naibu Spika, uzalishaji usio endelevu wa mkaa; Shughuli za kilimo; Biashara haramu ya mbao (illegal timber trading) na mkanganyiko katika sheria zinazosababisha degradation ya misitu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni vyema Serikali ikajipanga na kuja na mikakati mahususi na kuja na time plan itakayotumika kuboresha na kurekebisha changamoto hizi ili kuleta tija katika nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Maridhiano/Mikataba ya Kimataifa. Tanzania imeingia mikataba ya kimataifa kama, UN-CCD, Bonn Challenge, African Forest Landscape restoration, na Zanzibar Declaration kwa lengo mahususi la kuboresha soko la mazao ya misitu nje na ndani ya nchi, na kuhakilisha hali ya misitu nchini inaboreshwa. Ni nini status katika kutekeleza matakwa ya mikataba hii hapa nchini?

Mheshimiwa Naibu Spika, TFS Kuwa Regulatory Authority Kutoka Kuwa Agency. Kutekeleza hili kwa wakati itasaidia TFS na hivyo kujenga ufanisi katika kusimamia misitu yote nchini bila kuleta changamoto za mgongano wa kimamlaka.

Mheshimiwa Naibu Spika, Soko la Mbao Nje na Ndani ya Nchi. Tuna potential kubwa nchini katika sekta hii ila bado tupo nyuma sana kwani tunaendeleza biashara hii traditionally. Viwanda vingi nchini havi maximize recovery ya mbao na pia tupo nyuma katika grading ya mbao na kukosa fursa ya kujipatia fedha za kigeni. Kuna umuhimu wa kuviendeleza/kuvifufua viwanda vya mbao; kwa mfano viwanda vya Fiber Board-Arusha, Tembo Clipboard-Tanga.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kuhusu Soko la Mbao. Serikali ijikite katika kuongeza aina za mbao kutoka traditional types za mbao mfano, Mvule, Mkongo na Mninga na badala yake ku-diversity resources nyinginezo za aina za miti/miti mbadala.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna haja kwa Serikali kujitathmini katika suala la soko la mbao nje ya nchi kwani tunapoteza kama nchi mabilioni ya fedha za kigeni kutoka illegal traded timber Soko kuu la magendo limekithiri kwa malighafi nchi za Asia na hususan China. Ni nini status ya nchi baada ya kusaini The Zanzibar Declaration on Illegal Trade in Timber and Forest Products?

Mheshimiwa Naibu Spika, what is the status of community based forestry management and the commitment of the Government to uphold what it sets out in the forest policy of 1998? We are told there is draft revised policy, what is the current status and how rights of those depending on community forestry are being upheld?