Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Naibu Spika, hongera sana kwa kazi kubwa mnayofanya, tunaona mabadiliko makubwa katika kusimamia maliasili za nchi yetu, kazi mnaifanya, hongereni.

Mheshimiwa Naibu Spika, ombi, wananchi wa Kata za Nsenda, Uyumbu, Ugaila na Ukondamoyo zilizo Urambo zina malalamiko mengi kuhusu kupunguzwa kwa maeneo yao ambayo kabla ya mpaka mpya maeneo yalikuwa yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, tafadhari sana Serikali itatue migogoro ya mipaka na ikiwezekana warudi kwenye uhalali wa kuishi kule.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri, matangazo vivutio vyetu yaongezwe hasa nje ya nchi.