Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Gimbi Dotto Masaba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. GIMBI D. MASABA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba mchango wangu niuelekeze kwenye Sheria ya Fidia kwa Wananchi kipindi anapopata madhara ya kujeruhiwa na wanyama hususani mnyama aina ya tembo. Kwamba mwananchi akijeruhiwa na tembo analipwa fidia shilingi laki tano mpaka milioni na fidia hizo zinatolewa kwa wakati, jambo ambalo linasababisha usumbufu mkubwa kwa wananchi hawa. Hali kadhalika fidia ya mazao kwa wananchi kipindi mazao yao yanapoharibiwa wanarudishiwa fidia kidogo, ekari moja shilingi laki moja ilhali ekari moja ya kulima inakadiriwa kuwa laki moja, jambo ambalo si sawa, tunawapunja sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo ninaomba hii sheria ya fidia ibadilishwe kwani si rafiki tena kwa mazingira ya sasa kwani gharama za kilimo zinaongezeka kila siku na pia binadamu wanaongezeka lakini pia kutokana na kuwa na changamoto ya uharibifu wa tembo kuwa umekithiri, ni vizuri Serikali ikalitazama suala hili kwa undani zaidi ikiwa ni pamoja na kuchukua tahadhali zifuatazo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, moja, inasadikiwa miti ya pareto ni adui wa tembo , sasa kwa nini Serikali isianzishe kampeni ya upandaji wa miti ya pareto kwenye maeneo ya pembezoni mwa hifadhi ikiwemo na upandaji wa pilipili kwani pia pilipili ni adui wa tembo?

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha, ahsante.