Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, kuwekeza katika Utalii katika Jiji la Dar es Salam. Jiji hili bado halijatumika vizuri katika sekta hii, hasa utalii wa mji na maeneo ya kipekee. Mfano nyumba ya makazi ya zamani ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, jengo la Salamander, fukwe za bahari nakadhalika. Hii ni muhimu hasa kwa wageni wajapo Jiji la Dar es Salaam kutokea nchi za nje; mfano Jiji la Berlin Ujerumani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutengeneza ramani ndogo na mahsusi kwa maeneo ya kutembelea watalii, kwa mfano ramani mahususi ya Jiji la Dar es Salaam, kuonesha maeno na vivutio vya utalii. Kuongeza na kuboresha vivutio vya utalii Jijini Dar es Salaam, mfano Mto Msimbazi ukitengenezwa vizuri kuruhusu maji kupita wakati wote kwa kuboresha kingo na kuondoa takataka itawezesha matumizi ya boti na watalii wataweza kuzunguka kupita eneo hilo tutapata fedha lakini na mazingira yataboreshwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo yote yanayopita kwenye maeneo ya hifadhi yawe na matuta kwa ajili ya kuwakinga wanyama pori dhidi ya kugongwa na gari, kama inavyoendelea kwa sasa katika barabara ya Morogoro- Mikumi na Kitengule-Karagwe. Sheria na kanuni kali kwa watakaogonga wanyama katika maeneo ya hifadhi ya wanyama. Kuendelea kutangaza vivutio vya Utalii katika vyombo mbalimbali vya kimataifa kama CNN, BBC na hata kudhamini matukio muhimu duniani kama Olympic hata kwa kiwango kidogo kama Rwanda na PL League ya Uingereza.