Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, maliasili na utalii ni muhimu sana katika kukuza Pato la Taifa. Ili kukuza utalii Serikali inabidi kupunguza migogoro kati ya wananchi na Wizara. Kuna maeneo ya wananchi yamechukuliwa na Wizara, kwa mfano eneo la Iyegeya Kata ya Luhunga. Eneo hili limechukuliwa na hifadhi ilhali hakuna kitu chochote pale, wananchi hawana eneo la kulima na kufugia wanyama wao.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Serikali kuwarudishia wananchi maeneo ya Kitasengwa, Kata ya Mkangu, Ihomasa Kilolo, Kata ya Kasanga na Iyegeya Kata ya Luhunga. Maeneo hayo ni maeneo ambayo yapo ndani ya vijiji hivyo, wananchi wanakosa maeneo ya kulima ili kupata chakula na maeneo ya kufugia mifugo yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Mufindi tulikuwa na center ambayo ilikuwa kama chuo cha misitu ikiwa chini ya Wizara ya Misitu, sasa chuo hicho hakipo na mafunzo ambayo yalikuwa yakitolewa na Idara ya Misitu hayatolewi katika chuo hicho. Naomba Serikali kufufua Chuo cha Misitu Mufindi ambapo kuna shamba kubwa sana la misitu katika nchi yetu ya Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia naiomba Serikali kuendeleza kutoa misaada kwa vijiji ambavyo vinazunguka Msitu wa Sao Hill. Vijiji hivyo ni; Kata za Nyololo, Igowole, Mninga, Mtwango, Mninga, Luhunga na Mkungu. Kata saba, vijiji 42 ambavyo vipo katika Wizara ya Maliasili na walitoa ardhi kwa Wizara hii ili kupata miti ya mbao, sasa wananchi wakosa misaada ya kijamii kama ukosefu wa maji, vituo vya afya kwa Kata ya Mninga na Kata ya Mtwango.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana Wizara kuendelea kusaidia shughuli za kijamii. Napendekeza kuwajengea majengo ya kituo cha afya au zahanati na si kutoa fedha. Pia, kuwakarabatia miundombinu ya maji pamoja na barabara ili wananchi waweze kukuza uchumi wao.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naunga mkono hoja.