Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua nafasi hii kuipongeza sana Serikali yetu ya Awamu ya Tano kuanzia kwa Mheshimiwa Dkt. John Joseph Magufuli, Rais wetu, Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Naibu Waziri na watendaji wetu wote wa Wizara na mashirika yote ya umma na wadau wote. Shukrani hizi ni kwa ajili ya utendaji wake wenye dira kwa Watanzania wote.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa nitoe mchango wangu wa ushauri kwa Serikali yetu.

(a) Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ione umuhimu wa kutupatia mtumishi (afisa wanyamapori) kwa Halmashauri ya Mji wa Mbulu. Mnamo mwaka 2017 nilimuomba Mheshimiwa Waziri, Prof. Jumanne Maghembe kuhusu hali tete ya wanyama wakali waliopoteza maisha ya wananchi nane ndani ya miezi mitatu mwaka 2015. Nami niliandika barua Wizarani kuomba mtumishi walau mmoja, hata hivyo Halmashauri ya Mji wa Mbulu inapakana na Hifadhi ya Marang’, Manyara na Msitu wa Hifadhi ya NOWU, eneo lote hili lina wanyama wakali.

(b) Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara iharakishe fidia kwa wananchi walioharibiwa mazao yao kwa miaka ya 2016, 2017 na 2018 ambayo taarifa ya tathmini yao iko Wizarani (TANAPA).

(c) Mheshimiwa Naibu Spika, sheria itazamwe kuhusu viwango vya fidia na kifuta machozi kulingana na viwango vya sasa.

(d) Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba Serikali itoe fedha zinazoombwa na Wizara kwa asilimia 100 ili kuwezesha Wizara kutekeleza majukumu yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, naunga mkono hoja asilimia 100, naomba kuwasilisha.