Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nishauri Serikali kutoa elimu kwa vyombo vya habari na meseji kwenye simu kwa kuwa wananchi wengi wana simu ilikuwaelimisha faida za kupanda miti kwa matumizi ya kuni na mkaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, vitalu vile ambavyo vingi vilikuwa kwenye halmashauri zetu vinakufa kwa kukosa fedha za kuviendesha.

Mheshimiwa Naibu Spika, nishauri Serikali kutafuta njia mbadala wa mkaa kwani ukataji wa miti hautasimama mpaka njia mbadala; mfano gesi kuwa bei ya chini ndipo tutaweza kuokoa misitu yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kushauri Serikali kuboresha barabara zinazoingia hifadhini kuliko ilivyo sasa, barabara ni mbovu inatia aibu watalii wanapokuja kutembelea mbuga zetu mfano njia inayoingia mbugani.

Mheshimiwa Naibu Spika, hotel zetu nyingi zilizoko kwenye mbuga zetu haziko katika hali nzuri pia huduma zake si nzuri, Serikali ifuatilie.

Mheshimiwa Naibu Spika, nishauri Serikali kufuatilia au kuhakikisha inapunguza utitiri wa tozo uliopo tangu mtalii anapoingia nchini na kuelekea kwenye mbuga zetu ili kuwezesha watalii wetu kuvutiwa kuja nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, nishauri vyuo vyetu vya utalii vipitiwe, vingi havina sifa hivyo kutoa wahudumu ambao hawakidhi vigezo vya kimataifa, wengi hawawezi hata kuwasiliana kwa kushindwa lugha ya kiingereza hivyo kushindwa kuhudumia kulingana na mahitaji ya wageni.