Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Janeth Maurice Massaburi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. JANETH M. MASABURI: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kuwapongeza Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu watendaji wote na taasisi zilizoko kwenye Wizara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, moja, vivutio vyote vya utalii hapa Tanzania viwekwe kwenye website kwa kila Ofisi za Balozi zetu zilizoko nje ya nchi. Pili, kivutio kikubwa katika nchi yetu ni amani kwa hiyo ni jambo jema kutangaza nchi yetu kuwa ni nchi ya amani na ni mahali patulivu kwa kupumzika na kufanya utalii kwa utulivu mkubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia utalii, Wizara hii ishirikiane na Wizara nyingine kama Wizara ya Madini, Wizara ya Kilimo, Wizara Viwanda na Biashara na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki kwa pamoja tuweze kutumia Balozi zetu kutangaza rasilimali zetu kama utalii, madini, mazao, Kiswahili, amani yetu na mengine ambayo yatainua uchumi wa nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lugha mbalimbali zitumike kutangaza utalii kupitia channel yetu ya utalii, lugha kama Kichina, Kiarabu, Kijerumani, Kifaransa, Kihindi, Kirusi na kadhalika ili dunia yote iweze kuona na kuifahamu Tanzania kuwa ina vivutio na ni eneo zuri duniani na ni ya pili duniani kwa vivutio vya asili.

Mheshimiwa Naibu Spika, makapuni ya utalii ya ndani na nje yashirikiane kuitangaza nchi yetu kiutalii. Tuna upungufu katika sekta nyingi hasa zinazohusika na kutoa huduma mbalimbali ikiwemo eneo la hoteli. Huduma kwa mteja (customer care) mafunzo zaidi yatolewe kwa wafanyakazi wetu ili tuendane na ushindani wa kibiashara kwa nchi zilizotuzunguka kama Kenya, Rwanda na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kampeni kwa utalii wa ndani. Timu maalum ya Wizara na taasisi zake zifanye ziara maalum nje ya nchi na hasa maeneo ya Ulaya, Asia na Amerika kutangaza na kujifunza mbinu nzuri za kuongeza watalii kuja kwa wingi hapa nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.