Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza kazi nzuri. Naomba nitangulize kauli ya kusema kuwa naunga mkono hoja na pia niseme kuwa kwa kuwa mimi ni mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Wizara hii, mengi ya masuala ambayo ningependa kusema nimechangia katika taarifa yetu ya Kamati. Hata hivyo, naomba Waziri anipe ufafanuzi katika maeneo yafuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo ya Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori (WMAs); naomba ufafanuzi kuhusu suala la kucheleweshwa kwa mgawo wa fedha za WMA (za photographic safari na uwindaji) toka Serikali, sambamba ni vifuta jasho na machozi. Uchelewashaji huu unaathiri shughuli za utaratibu za uhifadhi na miradi ya maendeleo ya vijiji vilivyotenga maeneo yao yahifadhiwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba ufafanuzi kuhusu utaratibu usiofurahisha jamii wa usimamizi wa shughuli za uwindaji ni kwa nini Game Scouts wa WMA ambao wamekidhi vigezo vya usimamizi, ukaguzi wa utiaji saini vibali vya wawindaji. Hawapewi fursa hiyo watendaji na Idara ya Wanyamapori? Kwa nini wao ndio wasimamie uwindaji ndani ya eneo la WMA wakati Game Scouts walioelimishwa na wanaoaminiwa na jamii wapo? Tena hawa Game Scouts pia wanatambulika na Mkaguzi wa Idara ya Wanyamapori.

Mheshimiwa Naibu Spika, Jumuiya ya Wanyamapori Enduimet WMA inalalamikia Wizara ya Maliasili na Utalii kwa sintofahamu ya kushusha daraja eneo lao la uwindaji toka grade one kuwa grade two bila kuwashirikisha wala kuwafahamisha vigezo walivyotumia kuamua kitalu chao cha uwindaji cha Engasurai kushushwa hadhi.

Mheshimiwa Naibu Spika, athari za kushushwa hadhi kitalu hiki bila ridhaa ya wanajumuiya siyo tu kimewadhalilisha wenye jumuiya bali pia inawapunguzia mapato kwa zaidi ya 50%. Baya zadi ni kwamba Jumuiya ilishaingia mkataba na mwekezaji wa kitalu hiki kwa makubaliano ya kitalu cha daraja la kwanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, adha wanayopata baadhi ya wananchi kutokana na utaratibu unaotumiwa na vikosi vya kudhibiti ujangili kubaini wawindaji haramu. Katika wilaya yangu ya Longido nina orodha ndefu ya watuhumiwa wa uwindaji haramu ambao wamewekwa mahabusu magereza ya Arusha kwa zaidi miaka miwili sasa bila kesi zao kusikilizwa kila mara ni kutajwa tu na kurejeshwa magereza kwa madai kuwa uchunguzi unaendelea. Miongoni mwao wapo wa vijana wa umri mdogo ambao wamerubuniwa, ni watu wenye visa nao. Naomba Mheshimiwa Waziri aunde tume maalum ya kupitia tuhuma za mahabusu wote waliokaa muda mrefu magereza kwa tuhuma za uwindaji haramu bila kesi zao kusikilizwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kanuni za shoroba na maeneo ya mapito ya wanyamapori; napongeza juhudi za Wizara za kutenga masharoba ya kuendeleza uhifadhi katika nchi yetu. Hata hivyo, napendekeza juhudi hizo zishirikishe jamii zinazoishi katika maeneo hayo kwa karibu. Itapenda zaidi wakifanya matumizi bora ya ardhi na kupewa maeneo hayo wayasimamie wao wenyewe kama WMA au misitu asilia.

Mheshimiwa Naibu Spika, kubadili hadhi maeneo ya hifadhi; hii pia ni dhana yenye tija kwa uhifadhi wa mapori yetu isipokuwa nashauri yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, sheria za Wizara zinazokinzana zirekebishwe kwanza mfano TAMISEMI, Maliasili, Ardhi na Madini. Eneo la Ziwa Natron libaki ni ardhi oevu inayohifadhiwa chini ya jumuiya pendekezwa ya lake Natron WMA.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa haya machache, naunga mkono hoja.