Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Rose Kamili Sukum

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ROSE K. SUKUM: Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto na utatuzi wake; ukurasa wa 68–b-4-3 kutatua migogoro, Mheshimiwa Waziri napenda kujua ni jinsi gani utaweza kutatua migogoro ya Wafugaji na Watumishi wa TANAPA na wenye maeneo tengefu, kwani kumekuwa na sheria kandamizi kwa Wafugaji ambayo hutumika katika Wizara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, ng’ombe wakiingia kwenye hifadhi au game reserve, ng’ombe wanataifishwa, kutozwa faini kila ng’ombe Sh.50,000 hadi Sh.100,000, Mchungaji au mwenye Mifugo hutozwa Sh.300,000 au kifungo.

Mheshimiwa Naibu Spika, mfano, mfugaji aitwaye Wambura huko Serengeti alipigwa faini ya Sh.5,000,000, au kifungo cha miaka mitano (5) na kutaifishwa ng’ombe mia mbili tisini na nne (294).

Mheshimiwa Naibu Spika, Upande wa hifadhi ya Tarangire pia kupigwa faini wafugaji kila wakati na huo umekuwa ni utaratibu wa kila mara, Je, huo sio unyanyasaji kwa wananchi walio karibu na hifadhi hizo? Unyanyasaji huu umesababisha vifo kwa wafugaji kwa ajili ya kufilisiwa je, Mheshimiwa Waziri ataisaidiaje kupunguza adha kwa wafugaji wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vilivyozunguka Hifadhi kurejeshwa kwa wananchi kama vile Vijiji vya vya Gedamar, Gijedabung na Ayamango vilivyopo Wilaya ya Babati Tarafa ya Galapo, kwani Hifadhi ya Taifa ya Tarangire ina ukubwa wa kilomita za mraba 2,600 kwa Tangazo la Serikali la mwaka 1970, iweje mwaka 2010 kuwe na uwekaji wa beacon kwenye vijiji hivyo hapo juu? Ni vema kufanya uchunguzi wa hali ya juu kwa kuondoa huo uonevu kwa wananchi ambao wapo kwenye hivyo vijiji.

Mheshimiwa Naibu Spika, Tarangire National Park, Ruaha National Park, Rukwa Rwafi, Gurumeti Game Reserve, Ikorongo Game Reserve, Kijereshi Game Reserve na Maswa Game Reserve, baadhi ya Hifadhi za Taifa na maeneo tengefu yenye kunyanyasa wafugaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.