Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. JUMA OTHMAN HIJA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza natoa shukrani zangu kwako kwa kunipatia nafasi hii ya kutoa mchango wangu katika Wizara hii. Pili, napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri pamoja na watendaji wake wote kwa kutayarisha na hatimaye kuwasilisha katika Bunge lako Tukufu hotuba hii kwa ufanisi mkubwa. Katika kuchangia hotuba hii napenda kutoa mchango katika maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Idara ya Utalii; napenda kuipongeza Wizara hii kwa mikakati na matayarisho mazuri katika Idara hii ya Utalii. Hii ni Idara muhimu sana katika tasnia ya utalii. Ni idara ambayo inatakiwa iweze kupanga mipango mikakati ya kuongeza watalii nchini. Utalii ni miongoni mwa vyanzo vizuri katika nchi yetu, hivyo idara hii inafanikiwa kujua hilo na kulitafsiri kwa vitendo ili kufikia azma hii ya kuwa chanzo cha nchini katika nchi yetu badala ya kutegemea vyanzo vingine ambavyo havina uhakika.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu mwingine katika Idara hii ni kutayarisha mazingira ambayo watalii wanaokuja nchini waweze kufika katika vivutio vyetu vyote hasa vile vya Zanzibar. Zanzibar ni sehemu ambavyo vivutio vyake ni vya bahari na huku bara vivutio vyake vingi ni vya mapori, hivyo ni vizuri kuwaonesha watalii wanaokuja nchini vivutio vya aina tofauti vilivyopo kwenye nchi yetu ya Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.