Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi; nimshukuru Mwenyezi Mungu na niombe kuchangia Wizara hii kwa dakika hizo nilizozipata.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni kweli kabisa nikiri kwamba Wizara hii sasa hivi imepata majembe, tunaamini kabisa ni majembe ambao wanaweza wakafanya kazi yao sawasawa. Mheshimiwa Kigwangala kipindi umepata ajali ulikuwa kwenye mihangaiko yako hiyo ya kuhakikisha kwamba Wizara hii inakaa sawa, mwenyezi mungu akubariki sana na Mheshimiwa Naibu Waziri pia nimeshawahi kukuona Mtwara umekuja pale. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ya kwangu ni machache; jambo la kwanza; kwamba hiki kitabu cha hotuba ya Waziri, hii picha iliyowekwa hapa mbele ni picha ya jengo la kale lililopo mbele ya nyumba yangu pale Mtwara Mikindani. Jengo hili ni miongoni mwa majengo ambayo kimsingi yaani kama kweli Wizara ingekuwa na nia ya dhati ya kuhakikisha kwamba TTB inatangaza, inatangaza sawasawa vivutio hivi ambavyo vipo Mtwara Mikindani mimi naamini kwamba watalii wangemiminika wengi sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, jengo hili ni jengo ambalo lilitumiwa na Wakoloni na wakati huo jengo hili lilitumika kama Custom, kama magereza na kama ofisi zote za Serikali; yaani ofisi ya mkoa na ofisi ya wilaya vilevile ofisi. Kila kitu kilikuwepo ndani ya jengo hili ambalo liko kwenye picha hii. Jambo ninaloomba, Wizara ihakikishe kwamba sasa hivi kwasababu; tumekuwa tunaangalia hapa picha kwenye simu jana kuna dereva mmoja kamgonga mnyama twiga; twiga ni mnyama mpole sana. Sasa kwa sababu hawa wanyama wanagongwa gongwa, na pia mazingira na hali ilivyo hivi sasa hawa wanyama wataisha kwahiyo utalii utabaki kwenye mambo kale.

Mimi niiombe Serikali iwekeze kwenye kutangaza mambo kale. Mji wa Mikindani ni mji wa kipekee sana; Mheshimiwa Ngombale ameongea hapa, Mji wa Kilwa ni mji wa kipekee sana, una majengo mengi ya kale. Kama tukiamua kutangaza sawasawa TTB kafanya kazi yake tunaamini kwamba Serikali itaongeza idadi ya watalii. Tuanze na Mji wa Mikindani mji mkongwe wa mikindani ambao uko Mtwara Mjini.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo linguine, kuna fedha zinaitwa fedha za REGROW kazi yake ni kukuza utalii ukanda huu wa Kusini. Nilikuwa naomba kujua, nimekuwa nikizisikia fedha hizi kwa muda wa miaka minne hivi sasa. Hizi fedha zimeletwa ama zipo kwenye makaratasi tu? Kama zimeletwa kule kwetu kusini mkakati upoje? Kwa sababu kuchanganya, yaani leo hii watu wanavyosema kwamba Kusini wanazungumza Mbeya wanavyosema kusini wengine wanazungumza Morogoro. Kusini ni Mtwara na Lindi, kwamba kusini Kiserikali nchi hii ni Mtwara na Lindi. Kwahiyo tunataka Serikali kama fedha zimepatikana fedga za REGROW zije kutangaza utalii kusini Mtwara pale kwenye mji wa Mikindani, kule Kilwa Kaskazini na kule kwenye msitu ule wa Selou uliopo Lindi; tunaomba hizi fedha ziletwe kule. Isiwe inazungumzwa tu Iringa Kusini; watu wanazungumza Iringa wanazungumza Mbeya na Mtwara na Lindi mnaisahau. Kwa hiyo naomba hizi fedha za REGROW ziletwe kweli Kusini kwenyewe, kusini halisi ambako ni Mtwara na Lindi tunashida ya kutangaza vivutio vya kiutalii na kuboresha …

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: …katika mji wa Selous. Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine nilikuwa naomba nizungumze kuna hizi fukwe za bahari. Kuna fukwe za bahari kule kusini kuanzia pale Mnazi Bay Mtwara ni fukwe ambazo ni za Kimataifa, Wakoloni wote walipitia kwenye fukwe ya Mnazi Bay wakajenga mahema yao pale akina Vasco Dagama, akina nani na wengine wengi sana; wakaja mpaka Mji wa Mikindani wakajenga mahema yao pale. Hizi fukwe zimesahaulika; ni fukwe nzuri kuliko fukwe zote duniani; fukwe ya Mnazi Bay ipo, Mtwara Vijijini pale na Msimbati. Nilikuwa naomba Serikali kama imeisahau hii fukwe ihakikishe ya kwamba inatangaza hii fukwe; watu wa TTB waje kuiangalia hii fukwe kwa sababu Wajerumani wameweka kwenye page zao zote duniani; kwamba miongoni mwa maeneo ambayo wamepita maeneo muhimu ya fukwe muhimu Tanzania ni fukwe ya Mnazi Bay ambayo iko Mtwara Mikindani; naomba Wizara ije kuiangalia hii fukwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo nilikuwa naomba kujua; kuna suala la wauza mikaa. Wauza mikaa imekuwa ni kero sana kule Mtwara, wanakamatwa sana. Yaani mtu akishikwa na gunia moja na mkaa anapigwa sana na watu wa maliasili, ukiwauliza wanasema wanataka walipe ushuru. Sasa hawa wauza mikaa ni watu masikini kabisa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)