Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru sana kwa kunipa nafasi nami niseme machache katika Wizara hii ya Maliasili. Niipongeze Wizara; Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na timu yake, toka moyoni niwapongeze. Mimi ni Mjumbe wa Kamati, nafahamu kazi kubwa wanayoifanya na Wizara hii imetulia. Hongera sana na hongera pia kwa ushirikiano, maana yake Mawaziri wanapowapa ushirikiano watendaji maana yake mambo yanakwenda. Hongera mno na ndiyo maana Wizara hii sasa imetulia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme hili la Ngorongoro. Mheshimiwa Waziri ametuletea mchakato mzima ambao ulifanyika kwa mwaka mzima, tangu tarehe 23, Mei, 2018, ile timu aliyoiunda ya wataalam kuhusu Hifadhi yetu ya Mamlaka ya Ngorongoro. Nafikiri kwamba hata Kambi Rasmi ya Upinzani walikuwa hawana sababu ya kuandika katika ukurasa wa nane, kwa sababu Mheshimiwa Mchungaji, to be honest yeye ni Mjumbe wa Kamati, nilitegemea angempongeza kabisa wala asingeandika hiki cha Ngorongoro kwa sababu hatua ambazo zimechukuliwa na Serikali yeye mwenyewe anazifahamu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ombi langu kwa Mheshimiwa Waziri, wapitishe hiyo document mapema kwenye Baraza la Mawaziri, walete mapema tumalize mgogoro wa Ngorongoro ili mwisho wa siku ile hifadhi yetu tuiokoe. Kwa hiyo nimpongeze sana kwa hili ambalo wamelifanya na taarifa ameshaiandaa tunasubiri tu finishing.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia niwapongeze kwa Kamati hii ya Mawaziri ambayo Mheshimiwa Rais ameiunda na kazi inaendelea. Nafikiri ni vizuri sample size ikaongezeka, maeneo mengi hayajafikiwa kama ambavyo Wabunge wengine wamesema. Kuandaa hii taarifa ni jambo moja lakini naamini matatizo hayafanani; matatizo ya Tarangire na vijiji vile vitatu hayawezi yakafanana na maeneo mengine. Niombe kama taarifa hii sasa haijafanyiwa finishing, waongeze sample sizes zao ili vile vijiji ambavyo havijafikiwa viwe treated kwa maeneo yao na matatizo yao. Hilo naamini wanaweza wakalipokea maana ni concern ya Wabunge wengi.

Mheshimiwa Naibu Spika, la tatu ambalo nahitaji kuwapongeza ni suala zima la mchakato waliouanza wa kurekebisha Kanuni ya Fidia au Kifuta Machozi ya mwaka 2011. Nimekuwa nikilizungumzia hili kwa muda mrefu sana, nimwombe; kabla hajafikia finalization ya kanuni hizo waweze kufika Babati Mjini kuhusu wanyama ambao kwenye ile kanuni ya mwanzo walikuwa wanasema siyo wanyama waharibifu na siyo wakali, hawawezi waka-attack binadamu na boko wamekuwa kwenye kundi hilo, waje waone kwa sababu tuna watu zaidi ya 28 waliopoteza maisha, siyo kwenye Ziwa Babati tu, lakini wakiwa mashambani ambao wamekuwa attacked na wale viboko.

Mheshimiwa Nabu Spika, sasa niombe kabla hawajamaliza kanuni hizo, ambazo wako kwenye mchakato na nawapongeza, naomba wafike Babati waone waathirika na wahanga wa viboko ambao kwenye kanuni tunawa- define kwamba hawa hawana madhara na wananchi hawahitaji kufidiwa. Kwa hiyo kabla hawajamaliza niwaombe wafike ili tuone ni jinsi gani na hawa wahanga wanaweza kufidiwa. Nina majina yao nimeshapeleka ofisini kwao, tunafikiri kwamba sasa wana sababu ya kulitazama hilo kwa upya.

Mheshimiwa Naibu Spika, na la mwisho kwa siku ya leo nikuombe Mheshimiwa Waziri; Hifadhi ya Tarangire inafanya vizuri hata kwenye collection tunaona, kwenye mapato inafanya vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spia, lakini tuna mageti matatu, kuna geti la kibaoni kilomita sita kuingia Hifadhini ambapo watalii wengi wanatoka Arusha wanaingia hifadhini na kutoka. Pia tuna geti la Sangaiwe ambayo ina kilomita nane, vilevile tuna geti la Babati mjini Mamire to Tarangire kilomita
17. Nikuombe Mheshimiwa Waziri kupitia hifadhi ya Tarangire na Wizara yako muone jinsi gani ya kufanya maintenance ya malango yote haya matatu kwa sababu wakiingilia kibaoni Minjingu wakatokea geti la Mamire wakaingia Babati Mjini, ni mahali salama zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Babati tuna hoteli nzuri ambazo naona hata Dodoma hazipo, nzuri kabisa, lakini pia hali ya hewa Babati ni nzuri, tuna ziwa Babati ambako hata hao watalii Mheshimiwa Waziri wanaweza kuja kutazama hawa viboko. Pia tuna mlima Kwaraa ambapo pale watalii wanaweza wakapanda. Tuna maji ya moto Kiru, tuna maji ya mungu Singu na wakilala pale Babati inaweza ikawa exit yao kuja Kondoa kuangalia mambo mengine hapa Kondoa ambako mnayo kwenye Wizara yenu. Kwahiyo niwaombe mlitazame hili kwa upya, badala kutumia milioni 600 kwenye barabara ya kilomita sita ya Kibaoni tu mkatumia milioni 600 ku-maintain ni vizuri pia mka-maintain malango haya matatu…(Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisa kwa muda wa Mzungumzaji)