Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kunipa nafasi na kwa sababu ya dakika tano itabidi niende in a point form kwa sababu ni mjumbe muhimu sana katika Wizara hii. kwanza nianze kwa kuwapa pole ndugu zetu wa Pemba ambao ni wadau wakubwa katika utunzaji wa rasilimali hizi za Maliasili na Utalii wa Kisiwa cha Fundo ambao wamepata ajali jana mashua kama 34 zimepotea na tano hazijaonekana mpaka sasa hivi na watu zaidi ya 30 hawajulikani walipo. Kwa hiyo, wale Kasa na Makobe wanaowatunza kwa ajili ya Utalii na watalii watapata shida, kwa hiyo, tunawapa pole kwa tukio hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilisema mwaka jana wakati anachangia Wizara hii kumwambia Mheshimiwa Waziri kwamba ni Wizara moja ngumu sana ni Wizara yenye changamoto nyingi sana, ni Wizara ambayo inahitaji umakini mkubwa sana na nikamuonya Mheshimiwa Waziri kwamba asipokuwa makini anaweza kuwa ni Waziri atakayehudumu kwa muda mfupi. Lakini nitaanza kusema kwamba Mheshimiwa Waziri katika kipindi kifupi ameonesha umahiri na umakini na ameenda vizuri sana na haya mafanikio yanayopatikana sasa hivi basi ni kwa umahiri wake na kubwa zaidi au siri ya mafanikio yake ni ile namna anavyoshirikiana na walio chini yake na watalaam pamoja na wadau wa Sekta hii. Kwa hiyo, nikupongeze Mheshimiwa Waziri na timu yako kwa kufanya kazi vizuri. Niseme pia ni Mbunge nina miakasita humu Bungeni wewe ni Waziri wa nne katika Wizara hii tokea niingie humu lakini kwa uelewa wangu na nilivyoona nathubutu kusema kwamba ni Waziri bora kulikoni hao waliokutangulia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sisemi haya kwa utashi nasema kwa mifano. Kuna meli zaidi ya 12 za watalii za kitalii na watalii ambazo zimeingia katika kipindi hichi. Kuna Waisraeli 1000 wameingia hapa, Wachina 349, kuna kukuzwa hizi hifadhi za Biharaulo, Burigi, Kimisi, Ibanda na Rumanyika lakini kuanzishwa kwa Jeshi Usu vyote ni vitu ambavyo ni uthubutu wa Mheshimiwa Waziri pamoja na timu yake ambavyo ameweza kuvifanya, kwa hiyo, sisemi kwa utashi nasema kwa mifano ambayo iko wazi kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niache katika hilo kwa sababu ya muda niseme tu kwamba Mheshimiwa waziri ili tuweze kupata watalii wengi basi ni lazima kuna mambo lazima yatendeke, na kuna mambo Serikali lazima ijipange, wewe kama Waziri hutaweza ni mambo ya Kiserikali, Political stability transparent democracy hivi vitu lazima viwepo katika nchi, lakini pia kuboreshwa kwa miundombinu ya maji, umeme na barabara katika maeneo ya uwekezaji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kuwe na sheria na sera pamoja na kanuni za uwekezaji ili ziweze kuwavutia wawekezaji kuja kuwekeza katika nchi yetu. Kwa hiyo hatuna haja ya kuona watalii 2,000,000,000; 3,000,000,000 hiyo sio issue hoja ni kupata serious investors tukipata serious investors wakawekeza maana yake tutapawa watalii wa daraja la kwanza na daraja la pili na tukipata watalii wa daraja la kwanza na daraja la pili maana yake mtalii mmoja anaweza ku-spend from 1000 Dollars kwenda mbele, kwa hiyo, hata tukipata hao watalii 1,500,000 lakini watalii wenye maana ambao tuna serious investors wamewekeza basi tutaweza kupata fedha nyingi zaidi kulikoni kuwa na namba kubwa ya watalii lakini Pato dogo.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia watalii ili waje kwa wingi na wajirudia kuja na kuja kila mwaka lazima huduma zetu ziwe nzuri, kwa hiyo lazima uboreshe Vyuo vya Utalii ili vijana wetu waweze kusomeshwa na kuhitimu vizuri waweze kutoa service nzuri. Wageni wanaokuja wanakuwa na mila tofauti, tabia tofauti, madhehebu tofauti sasa ni sisi kazi yetu kuweza kuhakikisha kwamba tunawapatia huduma iliyo nzuri ili waweze kuja na mara nyingine tena. Kwa hiyo, lazima tuboreshe vijana wetu wasome.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu a muda nikuombe Mheshimiwa Waziri kuna sheria zinazokinzana sheria hizi zinahatarisha Maliasili zetu, kwa hiyo tukuombe kwamba Mheshimiwa Waziri uwe initiator ukae na Mheshimiwa Waziri wa Madini, Mheshimiwa Waziri wa Kilimo, Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Mheshimiwa Waziri wa Ardhi ili muweze kupitia sheria zote zile ambazo zinakinzana zinaleta ukakasi katika kutunza rasilimali zetu ili sasa tuweze kutunza. Mheshimiwa Waziri kuna sheria zinakinzana na zinahatarisha Maliasili zetu, hususani wanyamapori, tunakuomba katika hili basi wewe uwe initiator katika hawa Mawaziri muweke hiyo timu mupitie zile sheria na mlete hapa Bungeni ili tuzifanyie kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri …

NAIBU SPIKA: Kengele imeshagonga Mheshimiwa ahsante sana, sekunde 30.

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Naibu Spika, dakika moja tu. Niiombe Wizara ya Fedha hili suala la tozo zilizowekwa kwa ajili ya TANAPA basi ziondoshwe, kwa nini ziondoshwe kwa sababu TANAPA imepewa mzigo mkubwa sana inahudumia zaidi ya mbuga 11 sasa hivi ambazo hizo haziji nini na zimeongezwa na nyingine tano, sasa na hii fedha ambayo inakusanywa kama kodi inarudi kwa wananchi kupitia ujenzi wa barabara, shule na hospitali wakti TANAPA wanafanya kazi hiyo. Sasa kwa nini wakiingiza Magreda, Makatapila, Magari walipishwe kodi? Kwa hiyo naomba Wizara ya Fedha… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Yussuf, umeshaeleweka.