Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Spika, napenda kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Uvuvi; nishauri Serikali kuhakikisha kunakuwepo na meli za uvuvi kwa ajili ya kuvua katika vina virefu. Ilitokea wakati ambapo meli za kigeni zilivua samaki wakubwa katika kina kirefu na kupata samaki wengi na wakubwa. Hii inaonesha tulivyo na utajiri mkubwa katika bahari yetu inayotuzunguka.

Mheshimiwa Spika, nishauri Serikali kuongeza vifaa vya doria kwani maharamia baharini wako wengi hivyo kutushia uhai wa wavuvi katika bahari yetu.

Mheshimiwa Spika, Uhaba wa Viwanda vya Kuchakata Mazao ya Baharini. Ninaishauri Serikali kuhakikisha inawekeza katika viwanda vya kuchakata mazao ya baharini.

Mheshimiwa Spika, Mabwawa ya Kufugia Samaki. Wananchi wengi wanahitaji elimu ya ufugaji samaki katika mabwawa. Watu wengi wamehamasika sana juu ya ufugaji samaki lakini elimu hawana ya jinsi ya kutengeneza mabwawa na jinsi ya kuzalisha wa samaki.

Mheshimiwa Spika, Mifugo. Nipende kuishauri Serikali kuondoa uchapaji ng’ombe ambao unasababisha uharibifu wa ngozi, pia kupunguza thamani ya ngozi hizo na kukosa soko la kimataifa.

Mheshimiwa Spika, nishauri Serikali sehemu zilizo na mifugo kujengwa viwanda ili kuondoa adha hii ambayo inawapata wafugaji kupata masoko bora na rafiki. Usafirishaji kupeleka mbali imekuwa ni shida na ghali, hivyo kuwakatisha tamaa.

Mheshimiwa Spika, ninaishauri Serikali kuhakikisha inasimamia thamani ya nyama inayoliwa; mabucha mengi yanatoa huduma ya nyama isiyo salama kuanzia uchunaji hadi ukataji buchani.