Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE: Mheshimiwa Spika, pamoja na mchango kwa njia ya kuzungumza, naongeza kuchangia kwa maandishi.

Mheshimiwa Spika, nishauri juu ya uvuvi wa bahari kuu. Baada ya kuanzisha Shirika la Uvuvi (TAFICO), hakuna haja ya kusubiri kununua meli zinazomilikiwa na Serikali, waalike wawekezaji walio tayari kufanya kazi kwa kushirikiana na TAFICO. Walete meli zao, TAFICO ishirikiane nao tupate japo kidogo hicho tunachokosa. Serikali ipitie upya sekta ya uvuvi wa bahari kuu na kufanya maamuzi kwa mwongozo ulio sahihi.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeweza kudhibiti uvuvi haramu. Mafanikio ni kuwa samaki wameongezeka, wale wenye ubora unaotakiwa. Ushauri kwa Serikali ni kuwa Serikali inapaswa kuhakikisha kuwa uvuvi haramu haurejei tena. Eneo lenye mapungufu ni watendaji wa Wizara na idara za uvuvi, hawa ndio wanaohamasisha uvuvi haramu. Katika Mkoa wa Kagera maeneo ya visiwani, compliance iko juu sana ila sehemu za karibu na nchi kavu uvuvi haramu umeanza kurejea tena.

Mheshimiwa Spika, Niishauri Serikali Juu ya Sekta ya Maziwa. Sekta hii ni moja ya sekta zenye fursa kubwa ya kujenga uchumi jumuishi. Taarifa za wataalam wa sekta ya maziwa nchini Uganda wanasema Tanzania kwa uchache tuna fursa ya kuzalisha na kuchakata lita milioni nne kwa siku. Uganda kwa sasa wanazalisha na kuchakata lita milioni mbili kwa siku ukilinganisha na lita 150,000 kwa siku kwa nchi ya Tanzania.

Mheshimiwa Spika, ili Tanzania iweze kufikia kiwango hicho kwa kuazima uzoefu wa Uganda tunapaswa kufanya yafuatayo; moja, Serikali itenge maeneo sehemu za wafugaji nchi nzima kwa kuanzisha semi free range animal keeping. Wafugaji wasaidiwe kuendeleza maeneo hayo kupewa mitamba huku Serikali ikitegemea kupata uwekezaji wake kwenye maziwa yatakayouzwa.

Mheshimiwa Spika, pili, soko la maziwa ni kiwanda, viwanda vyote vya maziwa vipewe vivutio kadiri inavyowezekana. Punguzo/upotevu wa ushuru/tozo kwenye viwanda vitarejeshwa kutoka kwenye kipato cha wananchi na sekta za kuzalisha maziwa zitakazoshamiri.

Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia NARCO inaendesha zoezi la kugawa vitalu vya ufugaji Mkoani Kagera. Tatizo langu kwa zoezi hili NARCO na Wizara wanarudia makosa yaliyofanyika miaka ya 2005. Maamuzi ya Serikali ya mwaka 2005 juu ya ranchi za Mkoa wa Kagera tume nyingi ikiwemo ile ya makatibu wakuu sita ziliikataa. Tume ya makatibu wakuu sita iliundwa na Mheshimiwa Dkt. Magufuli akiwa Waziri wa Mifugo na hata akiwa Mkoani Kagera amekuwa akilaani ugawaji huu wa maeneo.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali katika zoezi hili izingatie yafuatayo:-

(a) Imalize migogoro ya ugawaji wa mwaka 2006, kwetu Muleba. Tunashauri vijiji vyetu vinne na vitongoji virudishwe kwa wananchi.

(b) Kabla ya kugawa maeneo, lazima wazingatie mahitaji ya vijiji jirani ambavyo hutegemea mbuga hizo kuchunga ng’ombe wao.

(c) Mkoa wa Kagera unahitaji na kutegemea sekta ya maziwa. Yatengwe maeneo mahususi kwa ajili ya wawekezaji waliotayari kujenga viwanda. Wawekezaji hao wapewe vivutio vya ziada kwani sekta hii inajenga uchumi jumuishi.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.